SUAMEDIA

Wafanyakazi SUA waaswa kushiriki Mashindano ya Chibunda CUP Msimu wa Sita kuimarisha Afya na Mahusiano katika kazi

 

NA: Nichorous Romani

Mashindano ya Michezo kwa Wafanyakazi wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) maarufu kama Chibunda CUP Msimu wa Sita yamefunguliwa rasmi leo tarehe 23/09/2022 katika Viwanja vya Michezo vya Kampasi ya Edward Moringe Sokoine mkoani Morogoro.

Prof. Samweli Kabote akimuwakilisha Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo Prof: Raphael Chibunda akifungua Mashindano ya Michezo kwa Wafanyakazi wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) maarufu kama Chibunda CUP Msimu wa Sita.

 Akifungua mashindano hayo Prof. Samweli Kabote akimuwakilisha Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo Prof: Raphael Chibunda amesema kuwa  mashindano hayo yanasaidia kuwakutanisha pamoja watumishi wa Chuo hicho  ikiambatana na kuimarisha afya zao ambapo itawasaidia kufanya kazi kwa ufanisi bila kusumbuliwa na magonjwa yanayosababishwa na mtindo wa maisha.

Pamoja na hayo Prof. Kabote ameongeza kuwa mashindano hayo yamekuwa yakifanyika kila mwaka na yamendelea kuwa na matokeo chanya kwa kuongeza mahusiano mazuri baina ya wafanyakazi na utendaji kazi katika chuo hicho.

Kwa namna ya kipee Prof. Kabote amewaasa wafanyakazi wote kutumia nafasi hiyo ya msimu huu wa sita kushiriki kikamilifu katika michezo yote na kila mmoja awe na hari ya kufanya mashindano hayo kuwa ni moja ya tukio katika Maisha yake kama mfanyakazi ikiwa na lengo la kumsaidia kumuweka sawa kimwili, kiakili na kuboresha mahusiano yake binafsi katika eneo la kazi.

Katika tukio hilo mara baada ya ufunguzi Michezo iliyoanza kutimua nyasi za viwanja vya Edward Moringe Sokoine ni Pamoja na  Mpira wa Miguu, Mchezo wa Kuvuta Kamba na Mpira wa Kikapu kwa wanawake, ambapo mashindano hayo yataendelea  mpaka kufikia kilele chake mwezi Octoba.







 

Post a Comment

0 Comments