SUAMEDIA

Wanawake SUA wafanya matendo ya huruma

 Na: Siwema Malibiche

Wafanyakazi wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) wamefanya matendo ya huruma kwa watu wenye uhitaji  iliyohusisha walemavu, wajane na wazee wasiojiweza wilayani Mvomero katika Kijiji cha Wami Sokoine.

Akizungumza katika tukio hilo, Mwenyekiti wa Kamati ya Wanawake Chama cha Wafanyakazi RAAWU Tawi la SUA Bi Enessa Mlay  amesema matendo hayo ya huruma ni matendo yanatoa nafasi ya kuwasaidia watu wasiojiweza wenye uhitaji na kwamba yana thamani kubwa kwa kusaidia na kuwafariji watu wasiojiweza.

Akizungumzia mambo ambayo yamefanyika katika matendo hayo Bi Mlaya  amesema wamepeleka nguo za aina zote zikiwemo nguo za kike na za kiume pamoja na nguo za watoto, chumvi, sukari, unga, sabuni na vitu vingine kutegemeana na jinsi wafanyakazi wa SUA wamejitokeza katika kufanikisha matendo hayo

Amewataka Wanawake kuwa na uangalifu mkubwa katika malezi ya watoto na wakisimamia mienendo sahihi katika elimu kwa watoto kwani kupitia elimu itasaidia kuzalisha wataalam bobezi na weledi watakaoisaidia Tanzania kupata maendeleo kupitia sekta mbalimbali iliwemo ya kilimo.


Kwa upande wake, Afisa Ustawi wa Jamii wilayani Mvomero Bi. Pelice Lumambo amewashukuru wafanyakazi wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo SUA kwa kuwatembelea na kutoa chchote walichonacho kwa watu wasiojiweza ndani ya Kijiji cha Wami Sokoine.

Naye Mkazi wa kitongoji wa Sokoine Kanisani Pili Hassan ambae ni miongoni ya  mmoja waliofikiwa na matendo hayo ya huruma amewashukuru wale wote waliojitoa kuwasaidia chochote walichojaaliwa na amewakaribisha wakati mwingine kutosita kuwatembelea Kwani wanajiskia faraja kuona kuwa Kuna watu wanawakumbuka na kuwajali.

Akizungumza katika tukio hilo Mwenyekiti wa Kitongoji cha Sokoine Kanisani Bw Omary Kapiato amewatoa hofu wale wote wanaoishi katika mazingira magumu kuwa kuna watu wanawajali na kuthamini  kama ambavyo Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo SUA  kimefanya kupitia wafanyakazi wake .

Matendo hayo ya huruma yamefanyika ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya sherehe za Siku ya Wanawake Duniani ambayo Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani kwa Mkoa wa Morogoro kimefanyika Machi 8 ,2025 katika Viwanja vya CCM Tangani Halmashauri ya Mji Ifakara yakiwa yamebeba kauli mbiu isemayo “Wanawake na Wasichana 2025: Tuimarishe Haki, Usawa na Uwezeshaji”



Post a Comment

0 Comments