SUAMEDIA

Usomaji ni kitu muhimu kwa Binadamu hasa anaposoma kitu chenye faida kwake na kwa Jamii

Na Nicolaus Roman

Imeelezwa kuwa usomaji ni kitu muhimu katika maisha ya kila siku kwa Binadamu hasa

anaposoma kitu chochote chenye faida kwake na kwa jamii jambo linaloweza kuleta maen

deleo kwa Taifa.

PICHA  KUTOKA MTANDAONI

Hayo yameelezwa na Bi. Editha Njau Msimamizi wa Kitengo cha Huduma ya Marejeleo

na Taarifa kwa Jamii katika Maktaba ya Taifa ya Kilimo iliyopo ndani ya Chuo Kikuu cha

Sokoine cha Kilimo (SUA) wakati akizungumza na SUA Radio kwenye kipindi cha Kapu

la Leo.

Amesema taarifa sahihi hupatikana kwa kusoma na kupitia machapisho mbalimbali

ambayo yameandaliwa kwa usahihi hasa na wataalamu yenye lengo la kuelisha kitu

chochote kile ambacho mtu anatarajia kupata matokeo chanya.

Bi. Editha amesema Maktaba ya Taifa ya Kilimo SUA ipo kwa ajili ya kumsaidia

mwananchi kufahamu mambo mbalimbali yatakayo mletea faida hususani katika kilimo,

uvuvi, usindikaji, biashara na ufugaji na lengo la machapisho hayo ni kuhakikisha mtanza

nia anapata taarifa sahihi na kuweza kuzalisha kwa tija.

“Ukiwa unasoma machapisho mbalimbali mara kwa mara utakuwa mbunifu katika eneo

lako ulilopo kwa sababu kumbuka yale machapisho yameandikwa na wataalamu baada tu

ya kufanya utafiti, hivyo wewe unapokuja kusoma unapata taarifa na maarifa, amesema Editha Njau

Aidha amesema ni muhimu kwa vijana kuwa na tabia ya kujisomea kwa kuwa

wanaposoma wanaongeza maarifa pia uwezo wao katika kufikiri unakuwa mkubwa na

utawapelekea kuwa wabunifu.

Kwa upande wake Msaidizi katika Kitengo cha Marejeleo na Taarifa kwa Jamii Bw.

Ismail Chibunda ambaye ni Msimamizi amesisitiza watu wote kuanzia watoto hasa

wakazi wa Morogoro wanatakiwa kuwa na utamaduni wa kujisomea kwa kuwa kwenye

kusoma ndio maarifa yalipo na Maktaba ya Taifa ya Kilimo iliyopo SUA ni kwa ajili ya

kila mtu si wanafunzi pekee.



Post a Comment

0 Comments