SUAMEDIA

Wazee waiomba Serikali kuwapatia Pensheni Jamii

 Na.Vedasto George/ Tatyana Celestine

Wazee Mkoani Morogoro wameiomba Serikali kuwapatia pensheni jamii kama ilivyo kwa wazee wa Tanzania visiwani Zanzibar ili waweze kujikimu katika maitaji yao muhimu ikiwemo malazi, afya na chakula pia kuwapatia wawakilishi wa wazee kwenye vyombo vinavyotoa maamuzi hapa nchini.

Mgeni Rasmi ambaye ni Mwakilishi wa Mganga Mkuu wa Morogoro  Dkt. Masumbuko Igembya akizungumza na Wazee wa Mkoa wa Morogoro katika Maadhimisho ya siku ya Wazee duniani yaliyofanyika Wilayani Mvomero Morogoro jana. (Picha na Tatyana Celestine).


Ombi hilo limetolewa na Wazee Mkoani Morogoro wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wazee duniani iliyo fanyika katika Tarafa ya Mvomero Kijiji cha Mvomero wilayani humo na kubeba kaulimbiu inayosema familia na jamii tuwajibike kuwatunza wazee.


Akisoma risala mbele ya Mgeni Rasmi Mwenyekiti wa Baraza la Wazee Mkoa wa Morogoro Samweli Mpeka amesema endapo serikali ya Tanzania itawapatia pensheni jamii itasaidia kuondokana na changamoto zinazo wakabili hususani za kimatibabu ambapo wawee wengi nchini ukosa matibabu yaliyo sahihi kutokana na kutokuwa na kipato. 

“Wazee wanao nufaika na pensheni ni wale tu walio  kwenya mfumo rasimi ambao ni sawa na asilimia 4 ya wazee wote asilimia 96 ya wazee wengine ambao wamelitumikia taifa la Tanzania  na kuweza kulipatia mafanikio na maendeleo  haya tuliyonayo sasa  kupita sekta isiyo rasimi  ya ajira binafsi ikiwemo kilimo,Uvuvi,Ufugaji  na biashara hawapati pensheni  ya haina yeyote”. Amesema Samweli Mpeka Mwenyekiti wa wazee mkoa wa Morogoro.

 Aidha Mpeka amesema licha ya serikali kuweka mipango mathubuti ya kuwalinda raia na mali zao lakini bado kundi hili limekuwa likikumbana na changamoto nyingi ikiwemo ukatili unaofanywa na baadhi ya wanajamii kwa kuwazulumu mali wazee kama mashamba na nyumba.

Nae mgeni aliyemuwakilisha Mganga Mkuu Mkoa wa Morogoro katika maadhimisho hayo Dkt. Masumbuko Igembya amesema katika Mkoa wa Morogoro  kuna wazee zaidi ya 100,000 (laki moja) huku wazee zaidi ya 40,000 (elfu arobaini) tayari wamepatiwa vitambulisho kwa ajiri ya matibabu  bure sawa na asilimia 31 pekee.

Kupitia Maadhimisho haya naomba kutoa rai kwa Wakurugenzi wote wa Halmashauri zote Mkoa wa Morogoro kuendelea na zoezi la kuwapatia vitambulisho vya matibabu wazee  hawa ivyo kila halmashauri iweze kujipanga  kwa kununua vifaa vyote vinavyosaidia kuweza kutoa vitambulisho ivi ili kila mzee ndani ya mkoa wetu wa Morogoro aweze kupatiwa kitambulisho”. Amesema Dkt. Masumbuko

“Lakini katika Mkoa wetu wa Morogoro  tumeendelea kuboresha Afya za wazee  kwa kutenga madirisha ya matibabu ya wazee na kuweka matangazo ya mpishe mzee apate uduma kwanza naili tumeweza  kulishuudia katika vituo vyetu vya kutolea uduma linatekelezwa kwa umakini mkubwa Kwa mwaka 2019 hadi mwaka 2020 jumla ya misamaha ya matibabu iliyotolewa kwa wazee kwa mkoa wa Morogoro ni zaiodi ya misamaha elfu 27”. Amesema Dkt. Masumbuko

 Katika hatua nyingine Dkt. Igembya ameongeza kuwa takwimu za kidunia zinaoyesha kwamba wazee wanaendelea kuongezeka ambapo sensa ya mwaka 2000 ilionyesha wazee kote duniani imefikia bilioni 1.9 nakusema ifikapo mwaka 2050 idadi hiyo itaongezeka zaidi na kufikia asilimia 23.5.

Awali akizungumza katika Kipindi cha Mchakamchaka cha suafm Naibu Rasi wa Ndaki ya Sayansi za Jamii na Insia Prof. Fatihiya Massawe amesema kuwa Chuo Kikuu cha Sokoine kimeona umuhimu wa siku ya wazee duniani kwa kuona mchango wao mkubwa katika ujenzi na maendeleo ya taifa hivyo kupitia ndaki hiyo wataendele kutoa elimu kwa wanajamii ili kujiandaa na maishaya uzeeni iwasaidie kukabiliana na changamoto wanazozipata wazee wa leo.

Vile vile ameongeza kuwa sua kwa kuungana na wadau wengine duniani imejitoa kushiriki katika kutoa taarifa stahiki kwa jamii hasa zinazohusu wazee na jamii kwa ujumla ili kuwajali,kuwathamini na kuwatunza wazee kama kauli mbiu ya mwaka huu inavyojieleza.

Siku ya wazee uadhimishwa kila mwaka na kutambuliwa na Umoja wa Mataifa kwa lengo la kuelimisha na kujenga hamasa kwa jamii katika kuboresha upatikanaji wa huduma na haki za wazee ili kuwa enzi.

 KATIKA VIDEO 


Post a Comment

0 Comments