Na Vedasto George
SUA
Serikali imezitaka Taasisi za Elimu Juu nchini kuakikisha zinaazisha programu za masomo ambazo zitaendana na vipaumbele vya kitaifa ili kuweza kuimarisha sekta mbalimbali ikiwemo ya Afya, Kilimo, Mifugo pamoja na Utalii.
Naibu katibu Mkuu Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknolojia Prof. James Mdoe akizungumza na Wathibiti Ubora Vyuo Vikuu hawapo pichani
Kauli hiyo imetolewa na Naibu katibu Mkuu Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknolojia Prof. James Mdoe mkoani Morogoro wakati akifungua jukwaa la siku mbili la wathibiti ubora vyuo Vikuu nchini (TUQAF) .
Amesema uanzishwaji wa programu zinazoendana na vipaumbele vya taifa zitasaidia kuzalisha wataalamu watakaoweza kuendesha na kusimamia miradi mikubwa ya kimkakati ikiwemo ya Kilimo, Afya, Mafuta pamoja na Gesi.
Aidha Prof. Mdoe amesema kuwepo kwa Idara ya Uthibiti Ubora katika vyuo vikuu nchini itasaidia kuimalisha Sekta ya Elimu, Uchumi wa Taifa pamoja na maendeleo ya jamii.
Wathibiti Ubora Vyuo Vikuu wakisikiliza mada mbalimbali
Akizungumzia dhamira ya kuwepo kwa jukwaa hilo Katibu Mtendaji Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania TCU Prf. Dominic Kiampa amesema kukutana kwa wathibiti ubora wa vyuo vikuu kwa siku mbili ni kujadili na kutathimini miongozo mbalimbali iliyotolewa na Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania na kuakikisha miongozo hiyo inatekelezwa ipaswavyo.
Kwaupande wake Makamu Mwenyekiti wa jukwaa la wathibiti ubora Vyuo Vikuu Tanzania (TUQAF) Kutoka Chuo Kikuu cha taifa cha Zanzibar IDDI ALI amesema wataakikisha wanatekeleza maelekezo yaliyotolewa na serikali katika kuakikisha sekta ya elimu inaimalika ikiwemo uchumi wa taifa.


0 Comments