Na: Asifiwe Mbembela
Baraza Kuu la Wafanyakazi wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) limefanya Mkutano wake wa 136 katika Ukumbi wa Baraza, Kampasi ya Edward Moringe, Morogoro.
Katika mkutano huo, wajumbe walipokea na kujadili taarifa mbalimbali pamoja na masuala yaliyotokana na Mkutano wa 135.
Aidha, Baraza Kuu lilipokea na
kujadili maendeleo ya utekelezaji wa Mpango Mkakati wa Chuo kwa mwaka wa fedha
2025/2026, kuanzia Julai 2025 hadi Machi 2026 pamoja.
Hoja na mapendekezo kutoka
mabaraza madogo na mikutano ya wafanyakazi kutoka maeneo mbalimbali 17 ya kazi
yalisikilizwa na kutolewa ufafanuzi na Menejimenti ya Chuo.
Mkutano huo uliangazia pia hoja
zilizokamilika ndani ya mwaka husika zikiwemo masuala ya kuboresha maslahi ya
wafanyakazi pamoja na maboresho ya huduma kwa wateja.
Aidha, Menejimenti ya SUA
ilitoa pongezi kwa wafanyakazi wote kwa ushirikiano wao katika kutekeleza
majukumu ya kila siku ya Chuo huku likiwatakia kila la heri wajumbe wa
kuchaguliwa wa Baraza la 136 ambao wamemaliza muda wao.
Kabla ya Mkutano huo wajumbe walifanya ziara ya kutembelea Miradi ya Chuo iliyopo Kampasi ya Solomon Mahlangu iliyopo Mazimbu na Kampasi Kuu ya Edward Moringe.
.jpg)






0 Comments