Na: Adam Maruma – Morogoro.
Serikali pamoja
na wa wadau wa maendeleo wametakiwa kumwezesha mwanaume kwenye harakati
mbalimbali za kiuchumi na kijamii ili
aweze kuwa nguvu na ushawishi katika jamii itakayomjengea kujiamini na
kuanzisha familia atakayoisimamia kwa faida ya jamii na taifa kwa ujumla.
![]() |
| Baadhi ya washiriki wa siku ya mwanaume Duniani wakiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya kuhitimishwa kwa Kongamano hio mjini Morogoro. |
Wito huo
umetolewa na Mhadhiri mwandamizi wa masuala ya Jinsia , sayansi ya jamii na maendeleo kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine cha
Kilimo SUA Prof. Rasel Madaha katika maadhimisho ya siku ya mwanaume wa kitanzania
iliyofanyika katika ukumbi wa Soko la Chief Kingalu uliopo Manispaa ya Morogoro.
Prof.
Madaha amesema kuwa harakati mbali mbali
zimekuwa zikimlenga zaidi mwanamke na kumsahau mwanaume ambae wakati mwingine
amekuwa na changamoto nyingi zaidi.
![]() |
| Mhadhiri mwandamizi wa masuala ya Jinsia , sayansi ya jamii na maendeleo kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo SUA Prof. Rasel Madaha akizungumza na Waandishi wa habari nje ya Kongamano hilo. |
Aidha
ameongeza kuwa kutokana na mabadiliko ya kiuchumi nchini na duniani kote
wanaume kama walezi na wasimamizi wa familia wamekuwa na changamoto mbali mbali
za kijamii na kiuchumi na hivyo kushindwa kuanzisha na kusimamia familia kama
ilivyo katika miaka ya nyuma.
Mhadhiri
huyo mwandamizi amesema kuna kila sababu
ya Serikali na wadau mbali mbali,kumwezesha katika harakati mbali mbali za
kiuchumi, na kijamii ili waweze kuinuka kuichumi.
Msomi
huyo wa masuala ya usawa wa kijinsia na maendeleo amesema jamii imakuwa na
dhana ya kumuona mwanaume kama mtu asiyehitaji msaada wowote,hali
inayowapelekea wanaume wengi kujikuta wakishindwa kupata misaada mbali mbali ya
kiuchumi na hivyo kubaki na changamoto ambayo huwapelekea wanaume wengi kupata
msongo wa mawazo na kufanya matukio ya ukatili wa kijinsia kwa wenza na watoto
wao au wakati mwingine kujiua wao wenyewe.
Kwa
upande wake Mhadhiri Mwandamizi kutoka Chuo Cha Mipango Dodoma Christina
Mandara, amesema siku ya mwanaume wa Kitanzania, ni siku muhimu ili kukumbusha
na kuifundisha jamii kuhusu kazi, majukumu na thamani ya mwanaume kwenye jamii
na familia kwa taifa kwa ujumla.
![]() |
| Mhadhiri Mwandamizi kutoka Chuo Cha Mipango Dodoma Christina Mandara, akizungumza na Waandishi wa habari mara baada ya Kongamano hilo. |
Ameongeza
kuwa mwanaume wa sasa bila kujali umri wao wamekuwa wakikabiliwa na changamoto nyingi
kutokana na mabadiliko ya kiteknolojia
na fursa za kiuchumi kwa wanaume na wanawake hali inayopelekea changamoto
mbalimbali za kimalezi.
Amefafanua
kuwa hali hiyo inayopelekea mabadiliko ya kimfumo wa kimalezi na ukuaji wa
mitandao ya kijamii pia imekuwa na changamoto zaidi kwenye eneo la malezi ya kwa
kufanya jamii kupata mafunzo yasiyo mazuri kwa jamii kupitia mitandao hiyo.
Nae Mhadhiri
mwingine Dkt. Jonas Gervas kutoka Chuo cha Ardhi katika wasilisho lake amewaomba wanaume
kugeuza changamoto mbalimbali zilizopo katika jamii kuwa fursa za ajira
akitolea mfamo wa namna taka zinavyoweza kuwa chanzo kizuri cha ajira kwa
kuzigeuza kuwa malighafi ya kutengeneza bidhaa mbali mbali kama mkaa na mbolea
kwa matumizi ya kilimo.
![]() |
| Mhadhiri kutoka Chuo cha Kikuu cha Ardhi Dkt. Jonas Gervas akifafanua jambo mbele ya Waandishi wa habari mara baada ya kongamano hilo. |
Amesema
kutokana na ongezeko la watu kumekuwa pia na ongezeko la uzalishaji wa taka
katika miji na majiji yenye idadi kubwa zaidi ya watu nchini kama Dar Es
Saalaam hivyo tafiti zinaonesha kuwa uhudumiaji wa taka hizo umekuwa changamoto
kwa halmashauri na majiji hivyo changamoto hiyo inaweza kuwa chanzo cha ajira
kwa wanaume kutokana na kuwa kumekuwa na viwanda ambavyo vinafanya
urejeshelezaji wa taka hizo kwa matumizi mingine.
Siku ya Mwanaume
wa Kitanzania imeadhimishwa kwa mwaka wa 3 tangu kuasisiwa kwake 2024 ambapo
kwa mwaka huu imeboreshwa zaidi kwa kuwa na usalishaji wa mada mbali mbali za
kitaaluma kutoka vyuo vikuu nchini kama Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo, SUA,
Chuo Kikuu cha Dar es salaam, Chuo cha Mipango Dodoma, Chuo Kikuu Ardhi, pamoja
na Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, huku washiriki wakijadili mada mbali mbali na
kubadilishana na uzoefu na kuongeza udadisi wa masuala ya usawa wa kijinsia ili
viweze kwenda pamoja na maendeleo jumuishi.
PICHA KATIKA MATUKIO NI BAADHI YA WASHIRIKI WA KONGAMANO HILO WAKIFUATAILI MADA ZINAZOWASILISHWA.









0 Comments