Na Vumilia Kondo
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeingia katika hatua ya lala salama ya kuhakiki Rasimu ya Taarifa ya Hali ya Haki za Binadamu nchini (UPR), itakayowasilishwa mbele ya Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa.
![]() |
| Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mheshimiwa Zainab Katimba akizungumza katika mkutano |
Akifungua kikao kazi cha uhakiki
wa rasimu hiyo mkoani Morogoro, Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mheshimiwa
Zainab Katimba amebainisha kuwa mchakato huo ni kielelezo cha utashi wa kisiasa
wa Tanzania katika kuheshimu utu na misingi ya kisheria.
Naibu Waziri ameeleza kuwa katika
mzunguko wa tatu uliopita, Tanzania ilikubali kutekeleza jumla ya mapendekezo
187, jambo ambalo ameliita kuwa ni ahadi ya kitaifa na kielelezo cha utayari wa
nchi katika kujitathmini.
"Taarifa mnayoandaa si
taarifa ya kawaida, ni taswira halisi ya namna Serikali inavyotekeleza wajibu
wake, uimara wa taasisi zetu na athari za kazi zetu katika maisha ya
wananchi."Amesema Mheshimiwa Katimba
Kwa upande wake, Mkurugenzi
Msaidizi wa Idara ya Haki za Binadamu kutoka Wizara ya Katiba na Sheria,
Richard Kilanga ametoa ufafanuzi wa kiufundi kuhusu mfumo huo akibainisha kuwa
huo ni mchakato wa kipekee ambapo nchi inafanyiwa tathmini na nchi wanachama
wenzake wa Umoja wa Mataifa.
![]() |
| Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Haki za Binadamu kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Richard Kilanga akizungumza na washiriki |
"Tanzania imekuwa ikishiriki
kikamilifu katika mchakato wa UPR tangu kuanzishwa kwake na sasa tupo katika
mzunguko wa nne. Katika mzunguko uliopita, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
ilikubali kutekeleza jumla ya mapendekezo 187." Amesema Richard Kilanga
Mkurugenzi msaidizi wa Katiba na sheria.
Ripoti inayohakikiwa sasa
imejikita katika maeneo ya kipaumbele ikiwemo uhuru wa kujieleza, ulinzi wa
maliasili za nchi, haki za watu wenye ulemavu hususan wenye ualbino, pamoja na
kuondoa ukatili dhidi ya wanawake na watoto.
![]() |
| Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mheshimiwa Zainab Katimba (katika) waliokaa akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa mkutano |
Mkurugenzi huyo ameongeza kuwa lengo kuu la UPR ni kuboresha hali ya haki za binadamu na kuleta matokeo makubwa kwa watu wote ulimwenguni, huku ikisaidia nchi kutimiza wajibu wake katika mikataba ambayo imeridhia.
.jpeg)

.jpeg)

0 Comments