SUAMEDIA

TPHPA kuimarisha huduma Njombe kwa kujenga maabara ya kisasa.

 Na: Mwandishi wetu - Njombe.

Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Mhe. Anthony Mtaka, amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Afya, Mimea na Viwatilifu Tanzania (TPHPA), Prof. Joseph Ndunguru.

Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Anthony Mtaka (wa kwanza kulia) akiwa na timu ya wataalamu kutoka TPHPA ikiongozwa na Mkurugenzi wake Mkuu Prof. Joseph Ndunguru (wa kwaza kushoto).

Lengo kuu la mazungumzo hayo likiwa kumkabidhi mkandarasi kwa ajili ya usanifu wa michoro na usimamizi wa ujenzi wa Maabara ya Kimkakati pamoja na jengo la utawala, ambayo yatajengwa katika Mji wa Serikali Lunyanywi.

Katika mazungumzo hayo, Prof. Ndunguru alieleza kuwa TPHPA imesaini mkataba wa kupeleka bidhaa 60 nchini Malawi, zikiwemo aina 30 za mazao yatakayosafirishwa huko.

Mhe. Mtaka alimshukuru Prof. Ndunguru kwa kutambua kuwa Njombe ni miongoni mwa mikoa inayozalisha chakula kwa wingi, hivyo kuna umuhimu wa kujenga maabara ya kimkakati itakayosaidia wakulima na wafanyabiashara kupata huduma bora za kisayansi na kiuchumi.

MATUKIO KATIKA PICHA WAKATI WA KIKAO HICHO.






Post a Comment

0 Comments