SUAMEDIA

Jaji Mfawidhi Morogoro awahimiza Wanawake kuchangamkia fursa za Dira ya 2050 na kuhakikisha malezi Bora.

 Na: Adam Maruma – Morogoro.

Imeelezwa kuwa wanawake kote nchini na duniani kwa ujumla wakipewa nafasi za uongozi kwenye Nyanja mbalimbali wanaweza na kusaidia jamii na taifa kupata matokeo chanya.



Hayo yameelzwa na jaji Mfawidhi wa Mahakama ya Morogoro, Mhe. Rose Eprahim wakati akizungumza katika kilele cha siku ya wananwake duniani kwa mkoa wa Morogoro kilichofanyika Tarafa ya Mikese kijiji cha Fulwe wilayani Morogoro.

Mhe. Jaji Rose alisisitiza kuwa wanawake si wahanga, bali wapo katika maeneo mbalimbali ya uongozi, uchumi na kijamii, na wanaendelea kufanya vizuri katika majukumu yao.

Aidha, aliwahimiza wanawake kuchangamkia fursa zilizopo katika Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050, akieleza kuwa wanawake wana jukumu kubwa katika kuifikisha nchi kwenye maendeleo yanayokusudiwa na hivyo kuwataka kuielewa vizuri Dira ya 2050 ili waweze kuitumia kama mwongozo wa kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya taifa.

Pia jaji Mfawidhi wa Mahakama ya Morogoro aliwataka wanawake kutumia vizuri nafasi na fursa wanazopewa na serikali kwani zimekusudiwa kuwainua kiuchumi na kijamii na hivyo kuwakumbusha wanawake kutoacha jukumu lao la msingi la kulea watoto katika maadili mema, kwani malezi bora ni msingi wa jamii imara.

Vilevile aligusia changamoto ya haki ya kumiliki ardhi, akisema bado imeendelea kuwa tatizo kwa wanawake wengi, hasa wajane, na hivyo akasisitiza umuhimu wa kuendelea kutoa elimu ya kisheria ili kuhakikisha wanawake wanapata haki zao ipasavyo.

 

Post a Comment

0 Comments