SUAMEDIA

Wataalam wa Cuba kufundisha Kihispania SUA kwa miaka miwili

 Na: Ayoub Mwigune

 Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kimepokea wataalam wawili wa lugha kutoka nchini Cuba, watakaofundisha lugha ya Kihispania kwa kipindi cha miaka miwili chini ya Idara ya Lugha, katika jitihada za kuendeleza elimu ya kimataifa na kuboresha umahiri wa lugha miongoni mwa wanafunzi. 


Akizungumza wakati wa hafla ya kuwapokea, Mratibu wa Kitengo cha Umaitaifishaji na Majalisi wa SUA, Prof. Jonathan Mbwambo, amesema ujio wa wataalam hao ni sehemu ya mwendelezo wa ushirikiano wa muda mrefu kati ya Tanzania na Cuba, unaolenga kuimarisha elimu, utafiti na urafiki wa kimataifa.

 Amesema SUA inatambua umuhimu wa lugha ya Kihispania katika mawasiliano ya kimataifa na inahamasisha wanafunzi kutumia fursa hiyo kujifunza lugha hiyo, ambayo ni miongoni mwa lugha zinazozungumzwa zaidi duniani.

 Kwa upande wao, wataalam hao, Bi. Yusimí Vigoa Maruri na Bw. Lázaro Nochea Vilella, wameeleza namna walivyo furahishwa na mapokezi mazuri waliyoyapata SUA pamoja na fursa ya kushirikiana na walimu na wanafunzi katika kukuza elimu ya lugha na tamaduni.

 Bi. Maruri amesema wamejipanga kuhakikisha wanafunzi wa SUA wanapata ujuzi wa kina wa lugha ya Kihispania na uelewa wa tamaduni za Cuba na Amerika ya Kusini, wakiamini kuwa ni msingi muhimu katika mawasiliano ya kimataifa na fursa za ajira duniani.

 






Post a Comment

0 Comments