Na: Farida Mkongwe
Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Musa Kilakala, amesema mabadiliko ya tabianchi yameendelea kuathiri kwa kiwango kikubwa ustawi wa jamii na mazingira, hivyo kuwataka wananchi kuacha tabia ya uchomaji moto kwenye milima, uharibifu wa vyanzo vya maji na kutofanya shughuli za kibinadamu katika maeneo yasiyostahili ili kulinda mustakabali wa mazingira.
“Msingi wa kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi ni elimu,
hivyo jamii nzima inapaswa kushirikiana katika kuelimisha wananchi ili wajue
athari za vitendo vyao kwa mazingira kwani jukumu la kulinda mazingira si la
Serikali pekee, bali ni la kila mmoja”, amesema Kilakala.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Uzamili, Utafiti, Uhaulishaji wa Teknolojia na Ushauri wa Kitaalamu ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Kongamano hilo, Prof. Japhet Kashaigili kutoka SUA, amesema kongamano hilo limeweka maazimio muhimu yatakayotekelezwa kwa vitendo.
Miongoni mwa maazimio hayo ni kuendeleza programu za
ubadilishanaji wa wanafunzi na walimu ili kujenga uwezo wa pamoja, kuanzisha
vituo vya teknolojia na ubunifu, pamoja na kuandika maandiko ya pamoja ya
utafiti yanayolenga kutoa suluhisho la changamoto za jamii.
Ameyataja maazimio mengine kuwa kongamano litachambua masuala ya kisera yanayohitaji kuwasilishwa serikalini, hususan katika maeneo ya afya, maji na mabadiliko ya tabianchi, ili kusaidia Serikali kuunda sera shirikishi zinazotokana na tafiti za kitaalamu.
Kongamano lijalo ambalo litakuwa la Tatu la Kisayansi la
Muungano wa Vyuo Vikuu Vitano litafanyika katika Taasisi ya Nelson Mandela ya
Sayansi na Teknolojia ya Afrika (NM-AIST) jijini Arusha.
.jpg)









0 Comments