SUAMEDIA

Teknolojia mpya ya "Soil Doc" yawezesha upimaji haraka wa afya ya udongo Nanenane 2025

 

Na: Hadija Zahoro

Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA), Idara ya Sayansi ya Udongo na Jiolojia kupitia Maabara ya Sayansi ya Udongo imekuja na kifaa cha maabara inayobebeka (Soil Doc) ikiwa ni teknolojia mpya inayorahisisha zoezi la upimaji wa udongo na kutoa majibu ndani ya muda wa takriban nusu saa.

Akizungumza na SUA Media katika banda la Afya ya Mimea, Mbegu na Udongo katika viwanja vya Nanenane Kanda ya Mashariki, Mtaalam wa Maabara ya Udongo, Dominica Mbawala, amesema kifaa hicho kinaweza kupima kiwango cha phosphorus na nitrogen mahali popote.

Ameeleza kuwa wanaweza kumpimia mkulima udongo kwa ajili ya maandalizi ya kilimo katika viwanja hivyo vya maonesho hayo na kumpatia majibu hapo hapo.

Kwa upande wake, Dkt. Hellen Kanyagha, Mtaalam wa Afya ya Mimea, ameeleza kuwa katika maonesho hayo ya Nanenane wapo kwa ajili ya kutoa huduma ya upimaji wa udongo, afya ya mimea na mbegu ambapo mkulima anapata huduma hizo hapo hapo bila gharama yoyote.

“Kwa sehemu ya udongo tumekuja na Soil Doc ambayo ina vifaa vyote vya kisasa ambavyo vinaweza vikapima kiasi cha tindikali, potassium, nitrate na virutubisho vingine vinavyopatikana kwenye udongo,” amesema Dkt. Kanyagha.






Post a Comment

0 Comments