Na:Josephine Mallango.
Wataalam
kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) wamebuni kilimo cha mjini cha
mboga mboga cha mapambo kisichotumia udongo ambapo wanafunzi wa sekondari
mkondo wa Amali kutoka Mafiga waliopo chini ya SUA wanashiriki katika kilimo
hicho kuanzia mwanzo wa uzalishaji mpaka
kuvuna.
Kilimo hicho cha saladi ambacho wataalam wa SUA wamekilima kwenye chombo chenye muundo wa pambo ambalo wengi wamezoea kuyaona katika maua, kinatumia maji, makumbi na vifuu vya nazi ambavyo vimesangwa na kuwa unga ambao unga huo unaweza kutengeneza mwenyewe nyumbani au kununua madukani kwa kilo sh. 4000/= tu.
Akizungumza
na SUA Media, Afisa Kilimo Mwandamizi kutoka SUA, Godwin Rwezaula, amesema
wamekuwa wakiwafundisha wanafunzi wa sekondari Mafiga mkondo wa Amali mbinu
shirikishi za kilimo cha mboga mboga mjini cha aina tofauti ikiwemo kilimo
hicho kisichotumia udongo kutokana na mazingira ukizingatia wanafunzi hao
wanatoka mjini.
Ameongeza
kuwa kilimo hicho kinafanywa hata sehemu isiyo na udongo kabisa kwenye nyumba
za kisasa za sasa zenye sakavu au vigae kwa kuwa hazichafui mazingira, ni
kilimo rafiki na safi ambacho pia kinatumia muda mfupi kuanzia siku 21 mpaka 30
unakuwa umevuna saladi yako, kinaokoa muda wa kupatikana kwa mboga za majani
nyumbani pia kinasadia kupunguza utapiamlo ambao unazikabili jamii nyingi.
Amesema lengo la kuanza na wanafunzi hao wa mkondo wa Amali kutoka Mafiga kuanzia hatua za awali za uzalishaji kwa vitendo inamjengea mwanafunzi tabia ya kuanza kuzalisha toka mdogo ili kumuwezesha kujitegemea na kuja kuwa mzalishaji mkubwa na kujiari mwenyewe badala ya kusubiri ajira, na kwamba kwa kipindi ambacho anasoma inampa hamasa ya kupata pesa ndogo ndogo za kujikimu.
Wanafunzi
wa kidato cha pili 54 kutoka shule ya sekondari Mafiga wamekuwa wakijifunza kwa
vitendo mbinu shirikishi za kilimo kutoka SUA ambapo Rwezaula amesema kilimo hicho kinaweza
kulimwa na mtu yeyote na kwamba wanashauri kabla ya kulima, kupata ushauri wa
kitaalamu na ujuzi ambao ni mwepesi ili kupata tija wakati wa mavuno badala ya
kulima kwa mazoea.
0 Comments