Na: Josephine Mallango
Mfumo huo kwa sasa umeanza kutumika kwa ng’ombe ambao huvalishwa kifaa maalum kwenye masikio, kinachosomwa kwa skana baada ya kupatiwa chanjo, taarifa zao zote huingizwa pamoja kwenye mfumo wa kidijitali unaoruhusu kusomwa kwa urahisi.
Serikali tayari imefanya uwekezaji kwa kuwapatia maafisa mifugo nchini vishikwambi pamoja na usafiri ili waweze kufika katika maeneo yote ya wafugaji kwa ajili ya kukusanya data.
Amesema pamoja na tafiti wanazoendelea nazo Maabara hii tayari imeshazunguka nchi nzima kuratibu na kubaini magonjwa ya mlipuko na majanga na kwamba maabara hiyo inayotembea ina uwezo mkubwa wa kupita katika maeneo yoyote hata maeneo korofi katika kipindi cha mvua.
Ameongeza kuwa magonjwa ambayo mpaka sasa yameshatambuliwa na maabara hiyo inayotembea ni pamoja na Mgumba mkoani Lindi, Marburg mkoani Kagera, homa ya nguruwe, sotoka ya mbuzi na kondoo (ugonjwa ambao dunia imeweka mkakati wa kuukomesha ifikapo mwaka 2030), homa ya Bonde la Ufa, Chikungunya na unyong’onyevu wa mifugo. Aidha, tafiti mbalimbali bado zinaendelea, ikiwemo ile ya kupe, kwa kukusanya sampuli kutoka maeneo tofauti nchini.
Akizungumzia miongoni mwa mafanikio, amesema kuwa Tanzania imepongezwa na Shirika la Afya Duniani (WHO) kwa kuweza kudhibiti ugonjwa wa Marburg uliolipuka mwezi Machi mkoani Kagera, ugonjwa hatari ambao mtu akiupata anaweza kufariki.
Hadi sasa ugonjwa huo umedhibitiwa na umekoma nchini, huku juhudi zikiendelea kupanua ushirikiano hadi kwa nchi za Korea na China, sambamba na kushirikiana na Maabara ya Taifa pamoja na wadau wengine wa ndani.
0 Comments