SUAMEDIA

SUA yapata Ushindi wa Pili Maonesho ya Nanenane Kanda ya Nyanda za Juu Kusini 2025

 Na: Mwandishi Wetu

Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kupitia Ndaki ya Kampasi ya Mizengo Pinda kimeibuka Mshindi wa Pili katika kundi la Taasisi za Elimu kwenye Maonesho ya Kanda ya Nyanda za Juu Kusini yaliyofanyika katika Viwanja vya John Mwakangale, jijini Mbeya.

Ushindi huu unaendeleza rekodi bora ya SUA katika kuonesha umahiri wake wa kutoa elimu yenye ubora wa kimataifa, kufanya tafiti zenye matokeo chanya na kuendeleza teknolojia bunifu zinazochangia maendeleo ya kilimo na kuboresha maisha ya jamii.

Kwa miaka kadhaa sasa, SUA imeendelea kuthibitisha nafasi yake kama taasisi bora nchini katika kuibua suluhisho za changamoto za kilimo na kuongeza thamani ya uzalishaji, sambamba na kuandaa wataalamu mahiri wa sekta hiyo muhimu.

Aidha, katika Maonesho ya Nanenane Kanda ya Mashariki yaliyofanyika mkoani Morogoro, SUA iliibuka Mshindi wa Jumla na Mshindi wa Kwanza katika kundi la Taasisi za Mafunzo na Utafiti, kutokana na mchango wake mkubwa katika sekta ya kilimo nchini.

Post a Comment

0 Comments