Na: Vumilia kondo
Tukio hilo limehudhuriwa na viongozi waandamizi wa Chuo, wajumbe wa baraza, na wadau mbalimbali, ikiwa ni ishara ya mshikamano na mwendelezo wa maendeleo ya Chuo.
Akifungua hafla hiyo, Mkuu wa Chuo Mhe. Jaji Joseph Warioba ametoa pongezi kwa Baraza la Chuo kwa Tathlitha ya 13 na hususan Mwenyekiti wake, Jaji Mkuu Othmani Chande, kwa usimamizi bora katika kipindi cha miaka nane iliyopita.
Amebainisha kuwa SUA imepiga hatua kubwa , si tu katika mafunzo na utafiti, bali pia katika maboresho ya mazingira ya kujifunzia na kufanya kazi.
“Ingawa rasilimali zetu ni chache, tumepata matokeo makubwa kupitia usimamizi makini wa Baraza,” amesema,Jaji Warioba.
Aidha amesisitiza kuwa elimu ndiyo chachu ya kuondoa umasikini na akahimiza mshikamano wa Baraza jipya na Menejimenti ya Chuo ili kuendeleza mafanikio.
Kwa upande wake Mwenyekiti Mpya wa Barazala la Chuo kwa Tathlitha ya 14 Andrew Massawe , amempongeza Jaji Mkuu Mstaafu
Mhe. Chande kwa mchango wake mkubwa katika kuimarisha SUA na kuahidi kuendeleza
kazi nzuri iliyoachwa.
“Katika zama hizi za sayansi na teknolojia, tunahitaji ubunifu,
mshikamano, na matumizi bora ya rasilimali ili kuhakikisha SUA inabaki kinara
wa ubora kitaifa na kimataifa,” amesema.
Naye Makamu Mkuu wa Chuo Prof. Raphael Chibuda ametumia nafasi yake kumshukuru Mhe.Jaji Mkuu Mstaafu Chande kwa uongozi wa mfano na kuwatambua wajumbe wote wa Baraza lililopita, kwa msaada mkubwa katika masuala ya ushauri na uratibu na wizara husika.
Aidha, amesisitiza kuwa nguvu mpya kutoka Baraza jipya zinapaswa
kuunganishwa na uzoefu wa wajumbe waliopo ili kuiwezesha SUA kusonga mbele.
Hafla hiyo imeacha alama ya mshikamano, heshima, na matumaini mapya kwa SUA kutokana na ushirikiano wa viongozi, wajumbe wa baraza, na wadau, Chuo kimepanga kuendeleza nafasi yake kama kitovu cha elimu, utafiti, na ubunifu kwa maendeleo endelevu ya taifa.
0 Comments