SUAMEDIA

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro atembelea banda la SUA, ahamasisha kilimo cha mjini

 

Na: Josephine Mallango 

 Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima ametembelea Banda la SUA na kutoa  hamasa ya shilingi  laki moja na kuwatafutia  masoko kwa kila mwanafunzi wa shule ya sekondari  Mafiga anayesoma mkondo wa Amali ambaye atalima bustani  ya  mboga, kilimo cha mjini kinachotumia mbinu shirikishi za kilimo bora cha mboga nyumbani kwa  kufuata teknolojia wanayofundishwa na SUA .

Mhe. Malima amefurahishwa na kilimo hicho ambacho kinatumia eneo dogo na vifaa vigumu  ambavyo vimeshatumika na kuwa  takataka zinazobaki baada ya matumizi badala ya kutupwa na kuchafua mazingira vifaa hivyo vinatumika kuzalishia mboga mboga kwa kutumia mbinu ya  udongo kidogo huku nyingine zikitumia makapi ya vifuu vya nazi vilivyosagwa na kupata unga unaopandwa mazao .

Mkuu huyo wa Mkoa amesema wanafunzi  hao wa mkondo wa Amali wanapaswa kujifunza kulima kilimo hicho cha mjini kwa vitendo kwa kuwa kitawasaidia katika matumizi madogo madogo ya kijamii ikiwemo matumizi ya mboga za nyumbani na pesa zao za kujikimu katika mambo madogo madogo ikiwemo kununua sabuni badala ya kuomba wazazi.

 


kwa upande wake mwanafunzi Kalunde  Khamis wa kidato cha pili amesema yeye amekuwa akilima nyumbani  mboga za maboga na mama yake ndiyo anamnunulia mbegu kutoka sokoni na kwamba anapenda kilimo kwa kuwa kinapunguza matumizi na kimewapa unafuu wa kupata mboga mboga badala ya kununua wanachuma nyumbani hapo hapo.

Naye  Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) Prof . Raphael  Chibunda amesema kwa sasa wanaangalia eneo kwa ajili ya wanafunzi hao wa sekondari kujifunza kwa vitendo ambapo kila mwanafunzi atalima mazao yake kuanzia hatua ya awali mpaka mavuno akisimamiwa na wataalamu kutoka SUA na kwamba mazao hayo yatakuwa  mali ya wanafunzi wenyewe ndiyo mmiliki siyo shule wala Chuo ili iwe motisha kwa wanafunzi hao .

 


Wakati huo huo Mhe. Malima ametembelea maabara  inayotembea ambayo imekuwa ikisaidia  Serikali pindi yanapotokea magonjwa ya mlipuko ambapo amesema maabara hiyo inayotembea kwa umuhimu wake anaona zingepatikana  zingine zaidi katika kila Kanda ili iwe rahisi pale inapotokea changamoto ya magonjwa  iweze kutatuliwa kwa haraka.











Post a Comment

0 Comments