SUAMEDIA

Ndaki ya Sayansi ya Jamii na Insia yajipanga kudahili zaidi ya wanafunzi 700.

Na: Siwema Malibiche

Katika kuelekea mwaka mpya wa masomo Ndaki ya Sayansi za Jamii na Insia, Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo imejipanga kupokea  wanafunzi  takribani 750  katika shahada zake 3 kwa muhula wa masomo 2025/2026.

Rasi wa Ndaki ya Sayansi za Jamii na Insia, Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo Prof. Samwel Kabote akizungumza kupitia SUA FM 101.1 Morogoro (Picha zote na Nicolaus Roma) 

Akizungumza katika kipindi cha Elimu na Taaluma kinachoruka kupitia SUA FM kuhusu udahili kwa wanafunzi 2025/2026,  Rasi wa Ndaki ya Sayansi za Jamii na Insia, Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo Prof. Samwel Kabote amesema idara hiyo inatoa shahada 3 na kuongeza kuwa Ndaki hiyo ina walimu zaidi ya  62 wenye vigezo stahiki kuhudumia wahitimu watakao wanaotarajiwa kujiunga na masomo hayo.

Amezitaja shahada hizo ni pamoja na  Maendeleo ya Jamii, Rasilimali Watu na Sheria za kazi,  na Mipango ya Maendeleo na Usimamizi  ambazo zimelenga kuwapa uwezo wanafunzi wa kujiajiri na kuajiriwa katika taasisi binanfsi na umma kwa kuleta maendeleo katika sekta mbalimbali nchini .

Mtangazanji wa SUA FM Adam Maruma akiendesha kipindi studio

Ndaki ya Sayansi za Jamii na Insia,  kutoka Chuo  Kikuu cha Sokoine cha Kilimo imeanzishwa 2015 ikiwa inatoa shahada moja   ambapo kwa sasa inatoa shahada  mbalimbali  zikiwemo shahada za umahiri na uzamivu tangu kuanzishwa kwake na  imekuwa ikiongezeka kutokana na mahitaji katika soko la ajira.

Post a Comment

0 Comments