Na: Hadija Zahoro
Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo
kimepata fursa za masomo na kubadilishana ujuzi na uzoefu kwa wanafunzi wake
wanaotamani kwenda kusoma nchini India.
![]() |
Udhamini huo unajumuisha Programu
mbili ikiwemo ya muda mfupi(ITEC) na Programu ya muda mrefu kwa wale
waajiriwa(ICCR) wakijumuisha nyanja ya sayansi ya akili mnemba.
Akizungumza na SUAMEDIA Mei
27,2025, Rasi wa Ndaki ya Tiba ya Wanyama na Sayansi za Afya Prof. Esron
Karimulibo amesema kuwa ziara hiyo iliyohusisha maafisa wa Ubalozi kutoka
nchini India iliongozwa na Bw.Rajnish Kummar,Mkuu
wa Mpango wa ITEC.
Prof.Karimulibo amesema kuwa
fursa hiyo haiihitaji kulipia chochote zaidi yakufanya maombi kwa njia ya
mtandao na wao watagharamia kuanzia tiketi, pesa ya kujikimu pamoja na pesa ya
ada ya masomo mara baada ya majibu kutoka.
![]() |
‘‘Kwahiyo naahidi mimi ndiyo
nimekabidhiwa majukumu na menejimenti kwahiyo nitahakikisha kwamba taarifa hizi
zinapatikana kwa wana jumuiya wote’’amesema Prof.Karimulibo.
‘‘Mimi natamani kuona
tunachangamikia fursa hizi kwa sababu huwa bahati haiji mara mbili kwa hiyo tunategemea
kwamba kadiri tutakavyokua tunapashana taarifa basi watu wazichangamkie’’ amesema
Prof.Karimulibo.
![]() |
Kwa upande wake Mkuu wa Mpango wa
ITEC, Bw.Rajnish Kummar amesema kuwa ana
matumaini kwa kile walichokijadili kitaleta mafanikio makubwa katika uhusiano
wao na SUA zaidi ya uhusiano wa kiuchumi, kifedha na sasa wanaanza kujenga uhusiano
huo kwa njia ya udhamini na kuahidi kuwajengea uwezo zaidi kwa kuhakikisha
wanapata elimu iliyojitosheleza.
Ameeleza kuwa watakaopata nafasi
ya kwenda kusoma nchini India,watafaidika kupata elimu bora zaidi na watapata
vyeti ambavyo vitawasaidia kusambaza maarifa yote waliyoyavuna nchini humo kwa
watu wengine wakiwemo wanafunzi, wanataaluma pamoja na watu wa kawaida.
0 Comments