SUAMEDIA

Wananchi mkoani Morogoro na mikoa ya jirani wameaswa kutembelea katika Maonesho ya Nanenane Kanda ya Mashariki

 Na: Siwema Malibiche

Wananchi mkoani Morogoro na mikoa ya jirani wameaswa kutembelea katika Maonesho ya Nanenane Kanda ya Mashariki yanayofanyika katika viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere kwa ajili ya kujifunza mambo mbalimbali yaliyomo katika sekta ya kilimo, mifugo na uvuvi kwa maslahi yao na taifa kwa ujumla.

                              

Wito huo umetolewa Agosti 4, 2024  na  Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Alexander Manyeti mara baada ya kumaliza kutembelea mabanda mbalimbali yaliyopo katika viwanja hivyo huku akisisiza kuwa  maonesho hayo yanatoa wigo mpana kwa wakulima kujifunza  na kubadili mifumo yao ya kilimo, ufugaji na uvuvi kwa maendeleo ya Taifa.

Amesema ameona jinsi ambavyo sekta binafsi wanaipenda nchi yao kwa sababu pamoja na kufanya kazi zao kibiashara wanatoa huduma kwa sehemu kubwa za kuwasaidia wafugaji, wavuvi na wakulima

                                

Vile vile Mhe. Mnyeti  amesema kuwa  kazi ya Serikali ni kuonesha njia, kusimamia na kuonesha mwelekeo katika sekta ya kilimo hivyo ni vizuri kwa taasisi za serikali kuwa mfano kwenye aina ya bidhaa wanazopeleka kwenye maonesho hayo kwa kuzingatia ubora wa bidhaa hizo.

Pia, amefurahishwa na aina ya teknolojia zilizooneshwa na wadau mbalimbali wa kilimo wanaoshiriki kwenye Maonesho hayo pamoja na halmashauri ambazo zitaendelea kukuza uchumi wa taifa na kuunga  mkono jitihada za Rais wa Samia Suluhu Hassan.

                                    

Aidha Mhe. Mnyeti  amezitaka taasisi husika kuendelea kutoa elimu kwa jamii ili kukuza uchumi na kutoa wito kwa wananchi  kuendelea kutunza mazingira ikiwemo misitu kwa kuepuka kufanya matendo yatakayo haribu mazingira kwa kufuata sheria zilizowekwa ili kulinda uoto wa asili.


 

 










Post a Comment

0 Comments