SUAMEDIA

SUA yawavutia wanafunzi kupenda kilimo kupitia Maonesho ya Nane Nane mkoani Morogoro

 Na, Winfrida Nicolaus

Imeelezwa kuwa Mafunzo kwa Vitendo pamoja na Tafiti zenye tija katika Sekta ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi zinazotolewa na Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo SUA kwa lengo la kumuwezesha kijana kuajirika na kujiajiri mwenyewe inaleta hamasa kubwa kwa watu walio wengi hasa vijana kutafuta fursa kwenye Sekta hiyo.

                                    

Hayo yamebanishwa na Mwalimu Emmanuel Mwakalibule kutoka Shule ya Upendo Amani iliyopo Kihonda Mtaa wa Kiegea A Manispaa ya Morogoro wakati alipotembelea Banda  la SUA kwenye Maonesho ya Nane Nane Kanda ya Mashariki katika viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere mkoani Morogoro  yaliyobeba kauli mbiu isemayo “Chagua Viongozi Bora wa Serikali za Mitaa kwa Maendeleo Endelevu ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi”.

Amesema maisha ya watanzania wengi yanategemea kilimo hivyo ni vyema kuwaelekeza vijana kwa vitendo waone na kutambua fursa mbalimbali zilizopo kwenye Sekta hiyo ili iwe chachu ya wao kuona umuhimu wa kilimo kwenye maisha yao na kukitumia kama fursa katika kuleta maendeleo yao binafsi na nchi kwa ujumla.

Mwalimu Emmanuel amesema wanafunzi wao wamejifunza katika  Banda la SUA ni zaidi ya matarajio yao kwakuwa wameona pia namna Sayansi ilivyo muhimu na namna ilivyo msaada kwa jamii hivyo wanauhakika wanafunzi wao wameelewa na kupata hamasa ya kujiunga na Chuo hicho na hilo ndilo wanalohitaji kwakuwa kilimo kina fursa nyingi zaidi inaonesha wazi elimu inayotolewa SUA itawapeleka moja kwa moja kwenye soko la ajira .

“SUA ni Chuo kikubwa kutokana na ubora wa kozi pamoja na Taaluma wanayoitoa imeleta chachu kubwa kwetu kutembelea Banda lao hata hivyo sisi kama walimu tumeangalia hali ya sasa ya soko la ajira lilivyo na mambo mengine yanayoendelea lakini pia Serikali inasisitiza kuwafundisha watoto elimu itakayowawezesha kujiajiri wao wenyewe na SUA ni mfano ulipo hai wa utoaji wa elimu hiyo”, amesema Mwalimu Emmanuel

Kwa upande wake Mwanafunzi Ashrafu Juma amesema amevutiwa sana na mafunzo ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi yanayotolewa na SUA kwa kuwa yanaonesha uhalisia wa nini Chuo hicho kinafanya kwa wakulima na kwamba amefurahishwa zaidi kuona uzalishaji wa Vifaranga vya samaki, ufugaji wake na mavuno yake kwa tija na kuelewa kuwa Kilimo kina faida kubwa endapo utakifanya Kitaalam.

Naye Erica Kimambo amesema amajifunza na kujionea shughuli mbalimbali zinazofamywa na SUA ikiwemo namna ya kufuga, kulima kilimo chenye tija lakini pia kuona bidhaa mbalimbali zitokanazo na  kilimo hivyo imempa hamasa ya kujiunga na Chuo hicho kwakuwa atapata elimu kwa vitendo itakayomuwezesha kutotegemea kuajiriwa pekee bali kuweza kujiajiri mwenyewe.

“Niseme niwaombe wanafunzi wenzangu kutoka shule zingine kuweza kuja kwenye maonesho haya katika Banda la SUA kujifunza kwa kuona kwa macho fursa zilizopo kwenye Kilimo, ufugaji na uvuvi lakini pia kupata elimu ambayo itawasaidia kuchagua fani zenye manifaa kwao”, amesema Erica Kimambo

 

                             



Post a Comment

0 Comments