SUAMEDIA

SUA yatoa mafunzo Bunifu kumuwezesha Muhitimu kujiajiri

 

Na, Winfrida Nicolaus

Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kupitia Idara ya Sayansi ya Lishe na Stadi za Mlaji Kitengo cha Ushonaji watoa mafunzo ya Bunifu mbalimbali ikiwemo kuviongezea thamani vitu vilivyopo kwenye jamii ambayo yanamuwezesha Muhitimu kuweza kupata fursa ya  kujiajiri mwenyewe.

                                        

Hayo yameelezwa Agosti 4, 2024 na Dkt. Zahra Majiri Mhathiri SUA wakati akizungumzia bidhaa mbalimbali zilizotengenezwa na wanafunzi wanaosoma kozi hizo katika Maonesho ya Wakulima, Wafugaji na Wavuvi maarufu kama Nanenane Kanda ya Mashariki yanayoendelea mjini Morogoro

                                 

Amesema katika maonesho hayo wameleta bidhaa mbalimbali ambazo zimebuniwa na kutengenezwa na wanafunzi wa kozi hiyo ambapo inaonesha jinsi wanafunzi hao walivyoongezea thamani vitu mbalimbali yakiwemo mapipa yaliyotumika na kugeuzwa meza na viti ambayo vinaweza kuwekwa kwenye bustani (garden), baa na hata kwenye migahawa hivyo wanayauza na kujiingizia kipato.

                            

“ Kama unavyoona hizi bidhaa zilizopo hapa haya yalikuwa ni mapipa tumetumia kama malighafi, haya mapipa mwanzoni yalikuwa yameshatumika lakini baada ya kutumika yanakuwa hayana kazi sasa ili yasiwe taka yakaongezewa thamani wakabuni kwa kuyakata katika miundo tofauti na kutengeneza meza na viti kama  unayoyaona”, amesema Dkt. Zahra Majiri

                               

Dkt . Zahra Majiri ameongeza kuwa wanazo bidhaa nyingine ambazo wanafunzi haohao wamezitengeneza ikiwemo batiki zilizotengenezwa  kwa kufuata viwango vyenye ubora kwakuwa azipauki wala kuchakaa haraka na kuna zile bidhaa zilizotengenezwa kwa mikono kwa kutumia nyuzi za aina mbalimbali na bidhaa hizo zinawakilisha utamaduni wa asili za kitanzania.

Amesema bidhaa zao ni tofauti na za watu wengine kwakuwa zimtengenezwa kwa viwango vyenye ubora unatakiwa na kuzingatia uhifadhi hivyo vinaishi kwakuwa vimetengenezwa kwa usahihi.
























Post a Comment

0 Comments