Winfrida Nicolaus
Chuo
Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kimepongezwa kwa kuifanya Kampasi ya Solomon
Mahlangu kuwa kituo cha mafunzo ambacho kinawasaidia vijana wa Kitanzania
kufikia malengo yao kitaaluma huku miundombinu ikiendelea kuhifadhiwa kwa ajili
ya historia na alama ya uhusiano wa kindugu, kirafiki na ushirikiano kati ya
Tanzania na Afrika Kusini.
Spencer Hodgson (kulia) na ujumbe wake alipotembelea Kampasi ya Solomon Mahlangu (kushoto) ni Dkt. Geoffrey Karugila Rasi wa Ndaki ya Solomon Mahlangu (Picha zote na Ayoub Mwigune) |
Amebainisha
hayo Bw. Spencer Hodgson mmoja wa wasanifu wa majengo na miundombinu wakati
harakati za ukombozi wa Afrika ya Kusini alipotembelea katika Kampasi ya
Solomon Mahlangu mjini Morogoro Juni 10, 2024 ambapo amesema sehemu hiyo ni ya
muhimu kwa maisha yao kwa kuwa waliishi katika eneo hilo.
Anasema
amefurahi kuona eneo hilo lililokuwa pori sasa ni sehemu ya Chuo Kikuu cha
Sokoine cha Kilimo, akisema wakati wanaondoka maeneo mengi yalikuwa wazi kwa
lengo la kuwasaidia kuona adui na kukimbia ambapo sasa eneo hilo limeboreshwa
na kuendelezwa katika historia.
“Nimefurahi
kuja Tanzania zaidi katika eneo ambalo lilikuwa sehemu ya maisha yangu,
nimetembea na kuona jinsi eneo lilivyoboreshwa zaidi kwa kujengea majengo
mapya, kupanda miti na kuitunza vizuri sehemu hiyo ya kihistoria inapendeza
sana hapa ndipo mahali tulipoanzia na baadaye kwenda Dakawa hivyo nasikia
fahari kuwa mahali hapa”, alisema Hodgson ambaye alikuwa sehemu ya wasanifu
majengo yaliyopo eneo la Solomon Mahlangu.
Naye mwenyeji
wake Dkt. Geoffrey Karugila kwa niaba ya Makamu Mkuu wa Chuo Prof. Raphael
Chibunda amesema kuwa ujio wa wageni mbalimbali kutoka Afrika ya Kusini
unaonesha dhahiri mahusiano mazuri baina
ya nchi hizo mbili akisema mahusiano hayo yanafanya SUA kuwa sehemu ya
kihistoria ambayo inaendelea kuenea siku hadi siku na kukitangaza Chuo.
“Spencer
Hodgson alikuja miaka ya 79 akiwa na familia yake huku binti yake akiwa na umri
wa miaka tisa (9) tu hivyo alisoma hapa kwa kuwa waliishi hapa hapo utaona ni
namna gani ujio wao umeweza kutusaidia kujua mambo mengi zaidi na ya faida ya
kutuwezesha kuendelea kuitunza sehemu hii ya kihistoria si hivyo tu wageni
wanapoendelea kuja chuoni kwetu tunajitangaza pia kwa kuwa sisi ni sehemu ya
historia hivo kwa kuwa tupo kwenye eneo hilo”, alisema Dkt. Karugila.
Ugeni huo
mbali na kutembelea majengo mbalimbali waliyokuwa wanatatumia kipindi hicho cha
kupigania uhuru kama Ukumbi wa Nelson Mandela Freedom Square pia wametembelea
makaburi ya Wapigania Uhuru wa Chama cha ANC.
0 Comments