SUAMEDIA

SUA itenge eneo maalumu kutatua changamoto ya Afya ya Akili - Dkt. Kweka

 Na: Tatyana Celestine

Menejimenti ya Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) inastahili kupogezwa kwa kuwa tofauti na mahala pengine kwa kuona umuhimu wa Mafunzo ya Afya ya Akili kwa wafanyakazi wote wa Kampasi za SUA na kuhakikisha wanapata uelewa wa kutosha  ili kukabiliana na changamoto zinazoweza kujiokeza wakiwa kazini na kijamii kwa ujumla.

                            

Amesema  hayo ikiwa ni siku ya pili ya mafunzo  ya Afya ya Akili  yaliyofanyika katika Kampasi ya Solomoni Mahlangu Mjini Morogoro Daktari Bingwa wa Figo kutoka Hospitali ya Rufaa ya Muhimbili Garvin Kweka   na kufanya wafanyakazi wa Chuo hicho wote kupata fursa  ya kujifunza kama matarajio ya Menejimenti ya chuo hicho ilivyotarajia.  

                         

Aidha ameomba Menejimenti ya SUA kuona umuhimu wa kuweka eneo maalumu chuoni hapo ambalo litamsaidia mfanyakazi kusikilizwa anapokutana na changamoto za kihisia, kimwili, jamii ,dini na akili kutokana na uhalisia wa matatizo ya namna hiyo kuongezeka kwa kiasi kubwa nyakati za sasa nchini kutofautisha na zamani hivyo kwa kutumia muda wa kujifunza mara kwa mara na ukaribu utasaidia kupunguza madhara yatokanayo na tatizo la Afya ya akili.

                        

Daktari huyo amebainisha kuwa watu wengi wanatafuta akili za darasani zaidi intelligence quotient (IQ) na kusahau akili hisia Emotional intelligence (EQ) ambapo ni chanzo cha kuharibu kila kitu katika safari ya kutafuta mafanikio kwa mwanadamu hivyo ili waweze kufanikiwa wanatakiwa kuzingatia vyote kwa pamoja nayo itawafanya wasijitenge na jamii zaidi kuweza kutumia fursa mbalimbali hata kugeuza matatizo kuwa fursa na kuachana na msongo wa mawazo ambao hatma yake ni kuibua tabia zisizofaa, kutojipenda, kujiua na kupoteza hali ya uwoga pasi kuzingatia dini, tamaduini na malezi.

                                 

Dkt. Kweka ameendelea kufafanua mambo matano ambayo mfanyakazi anatakiwa kuyazingatia ili kuweza kuishi na mtu yeyote na kusema kuwa mambo hayo yana msaada mkubwa kwao na wateja wao kwani watatambua namna ya kusoma hisia za kila mmoja na kubadili njia ya kuweza kusikilizwa au kumsikiliza mtu mwenye changamoto ya afya ya akili na kuyataja mambo hayo ikiwa ni pamoja na kuzuia,kupokea,kubadili muelekeo, na kukubali.

                                

Ameongeza kuwa kati ya mambo hayo matano, matatu hayapatikani darasani bali katika jamii tathmini zinaonesha wafanyakazi wa leo wanakosa vitu vingi katika jamii kwakuwa wamejiwekea mkakati wa maisha yao kwamba wanatakiwa wakitoka kazini kuelekea kanisani ama msikitini  kurejea nyumbani bila kujali jamii inayowazunguka ambayo haihitaji gharama kubwa kuweza kuifikia zaidi ya ukarimu na kushirikiana nayo katika mambo ya kijamii tabia inayopelekea wafanyakazi kukosa msaada wa haraka wanapokuwa hawapo nyumbani.

                               

“Binadamu ukimfungia ndani unambadilisha hali ya afya yake ya akili anapata mihemko isiyokuwa sahihi, hivyo ili kuweza kukabiliana na msongo wa mawazo mahusiano na jamii ni sehemu muhimu ya afya ya akili” Amesisitiza Dkt. Kweka



                             

















Post a Comment

0 Comments