SUAMEDIA

Wafanyakazi SUA wapatiwa uelewa kuhusu Afya ya Akili

 

Na: Tatyana Celestine

Ili kuhakikisha wafanyakazi wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) wanapata uelewa kuhusu Afya ya Akili kutokana na kuwepo kwa changamoto hiyo nchini Menejimenti ya Chuo imeamua kuwapa mafunzo ili kukabiliana na hali hiyo katika utendaji wa kazi wa kila siku pamoja na maisha kwa ujumla.

                

Muwezeshaji katika mafunzo hayo Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Figo, Dkt. Garvin Kweka kutoka Hospitali ya Rufaa ya Muhimbili jinini Dar es salaam amesema kuwa wafanyakazi wanahitaji elimu hiyo ili  kujitambua na kufanya kazi kulingana na mazingira na kukabiliana na changamoto mbalimbali wanazokutana nazo ikiwemo afya, hisia, jamii na malezi ya watoto.

                 

Ameongeza kuwa matatizo ya afya ya akili yamekuwa kwa kasi kutokana na ukuaji wa sayansi na teknolojia na kufanya mambo mengi kubadilika na kupelekea binadamu kushindwa kuhimili changamoto zinazowakabili na matokeo yake wanafanya maamuzi ya  kujiua, kujiingiza katika mambo yasiyofaa kama uvutaji shisha, unywaji pombe uliopitiliza, ulaji mbaya vitu ambavyo kupelekea kupata magonjwa yasiyoambukizwa ikiwemo Kisukari na Msongo wa Mawazo hatimaye kifo.

                

Dkt. Kweka amewataka wafanyakazi kuwa wawazi kwa watu  wanaowaamini kwani sayansi inasema ili kutibu matibabu ya afya ya akili asilimia 80 ni kuongea hivyo njia hiyo itawasaidia kutatua changamoto zao pamoja na kuacha tabia ya kujitenga na jamii kwani kupitia jamii ufumbuzi wa changamoto hupatikana  kabla na baada ya kustaafu.

Mafunzo hayo yatatolewa katika Kampasi zote za SUA ambapo yameanza na Kampasi Kuu ya Edward Moringe Sokoine, Solomoni Mahlangu na baadae kuelekea Kampasi ya Mizengo Pinda iliyoko mkoani Katavi.

                                  











Post a Comment

0 Comments