SUAMEDIA

SUA Chuo pekee kinachotoa elimu bora kwa gharama nafuu Afrika

 

Na: Tatyana Celestine

Katika kuhakikisha ushirikiano na mawasiliano mazuri kati ya wanafunzi wa ndani na nje ya nchi wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kimeamua kupunguza gharama za Ada kwa wanafunzi wa kimataifa na kufanya SUA kuwa Chuo pekee kinachotoa elimu yenye ubora kwa gharama nafuu Afrika kwa lengo la kuendelea kuvutia watu wote duniani kujiunga na Chuo hicho.

                        

Akizungumza na wanafunzi kutoka mataifa mbalimbali katika Siku ya Kimataifa ya SUA kwa niaba ya Makamu Mkuu wa Chuo Prof. Raphael Chibunda, Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Taaluma, Utafiti na Ushauri wa Kitaalam Prof. Maulid Mwatawala amesema wanafunzi wote katika Jumuiya ya Africa Mashariki wamepata punguzo la Ada kwani  wameamua kutoa elimu bila kujali utaifa na kuendelea kufanya Chuo hicho kuwa na hadhi ya kimataifa kwa kuweka miundombinu rafiki kwa wote wanaopata nafasi ya kusoma hapo.

                                    

Prof. Mwatawala amesema  Chuo kinaendelea kuimarisha ubora  wa elimu kwa kupitia mitaala na kufanya elimu inayotolewa chuoni hapo kuwa kwa vitendo zaidi pamoja na kuhakikisha mahitaji muhimu ya wanafunzi wote yanapatikana kikamilifu ili waweze kuishi vizuri wawapo chuoni kwani nchi ya Tanzania ina makabila zaidi ya 24 hivyo amewataka wanafunzi hao kutumia fursa hiyo kwa kujifunza Kiswahili wasichukulie hiyo kama ni changamoto kwao bali fursa na hiyo ndio maana halisi ya kimataifa.                                                                            

Kwa upande wake Mratibu wa Umataifishaji na Majalisi SUA Dkt. Jonathan Mbwambo amesema kuwa siku hiyo ya kimataifa SUA wao wanaitumia kwa kuwaweka pamoja na pia kusikiliza changamoto za wanafunzi wa kimataifa ili kuendelea kuboresha maisha ya wanafunzi kitaaluma na kawaida ambapo wataonesha mila na desturi kutoka mataifa mbalimbali ambapo SUA inatumia fursa hiyo  kujitangaza kimataifa.

                                

Naye Mwanafunzi wa kimaifa kutoka Zimbabwe Nqobizitha Mpofu amesema hajawahi kujuta kujiunga na SUA kwani elimu na mazingira rafiki ya chuo hicho kwa upande wake SUA ni namba moja Afrika katika kutoa mafunzo ya kilimo kwa ubora kwani tangu amewasili hapo amejionea wakufunzi wakifundisha vema na hakuna changamoto yoyote waliyokutana nayo.

                                                                   

Vilevile Mwanafunzi wa mwaka wa nne Kozi ya Tiba ya Wanyama  Bi. Jtumbisa Tjijembo kutoka Namibia amesema Menejimenti ya SUA inajitahidi kuwafanya waishi vizuri wakiwa chuoni hapo na hata kuwaandalia siku kama hiyo inayowakutanisha kwa maana inaashiria Afrika ni wamoja yeye binafsi kupitia chuo hicho kimemjenga kuona hakuna jambo linaloweza kuwa gumu kutokana na kuchanganyika watu kutoka mataifa tofauti na kuishi vizuri.

                                        

Kupitia siku hiyo mataifa mbalimbali yameweza kuonesha tamaduni zao kwa mavazi, kuelezea historia ya mataifa yao, chakula, pamoja na kufurahia nyimbo za kitamaduni ambapo wanafunzi 105 wakiwemo kutoka Nchi ya Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Lesotho, Comoro, Zimbabwe, Mauritius, Afrika ya Kusini, Botswana.

                            

Nchi nyingine ni Kongo, Liberia, Ethiopia, Eswatini, Namibia, Congo, Berlin, Nigeria na Mozambique  yameweza kuonesha namna wanavyoweza kucheza na kupika vyakula vya utamaduni wa mataifa yao.













Picha zaidi bofya hapa chini


Post a Comment

0 Comments