SUAMEDIA

Wiki ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu kufungua fursa kwa wananchi, watafiti na wabunifu

 Na: Gerald Lwomile

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Carolyne Nombo amesema Wiki ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu 2024 itajenga uelewa na kufungua fursa nyingi kwa wadau mbalimbali wa Sekta ya Elimu nchini.

Prof. Carolyne Nombo akizungumza na waandishi wa habari  katika viwanja vya Popatlal Tanga (Picha zote na Gerald Lwomile)

Prof. Nombo amesema hayo leo Mei 26, 2024 katika viwanja vya Shule ya Sekondari Popatlal jijini Tanga, na kuwa watu watapata taarifa za vyuo mbalimbali wanavyoweza kujiunga na wabunifu wa teknolojia watauza kwa kuzitangaza bidhaa zao.

Prof. Nombo amesema kumekuwa na teknolojia nyingi zilizozalishwa na vijana ambao wanasoma katika vyuo mbalimbali nchini, ambazo zimekosa jukwaa la kuzionyesha na namna zinavyoweza kutatua changamoto mbalimbali hivyo kupitia wiki hii ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu watapata fursa ya kuzionyesha.

Afisa Udahili kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo  Bw. Ally  Ramadhan (kushoto) akitoa maelekezo ya namna ya kufanya udahili mtandaoni.

Aidha Prof. Nombo amesema kuna wabunifu wengi nchini ambao wanapata malezi kutoka Tume ya Sayansi na Teknolojia Tanzania watakutanishwa na wadau mbalimbali ili kubyasharisha teknolojia na ubunifu wao ili uweza kuingiza kipato kwa mtafiti au mbunifu na taifa kwa ujumla.

Naye Ramadhan Shedoe na Leah Kavishe ambao ni wakazi wa jijini Tanga wameimbia SUA Media kuwa maonesho hayo mbali na kuwaletea ujuzi na ubunifu kutoka maeneo mbalimbali lakini pia yananyanyua uchumi wa Jiji la Tanga.

Bi Leah amesema imekuwa faraja kubwa kwa wakazi wa Tanga kupata fursa ya kujua ni wapi wanaweza kupeleka watoto wao kwa mafunzo ya elimu ya juu na elimu ya kati.

Picha chini ni matukio mbalimbali katika banda la SUA










Post a Comment

0 Comments