SUAMEDIA

SUA kuendelea na tafiti ili kufikisha teknolojia na taarifa kwa kutumia Akili Mnemba

 Na: Gerald Lwomile

Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kimesema kinaendelea kufanya tafiti mbalimbali ikiwemo matumizi ya Akili Mnemba ili kurahisisha mawasiliano na upatikanaji teknolojia za kilimo na taarifa sahihi zinazoweza kuwasaidia wakulima katika kutatua changamoto zao.

Joseph Ruboha Mhadhiri Msaidizi na mbobezi katika fani ya wadudu kuitoka Kampasi ya Katavi ya Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo akitoa maelezo juu ya Nyuki (Picha zote na Gerald Lwomile)

Hayo yamesemwa Mei 25, 2024 na Mkuu wa Kitengo cha Ugani kutoka Taasisi ya Elimu ya Kujiendeleza ICE – SUA Dkt. Emmanuel Malisa katika maonesho ya Wiki ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu yaliyoanza jijini Tanga.

Dkt. Malisa amesema matumizi ya Akili Mnemna na mawasiliano rahisi yakiwa ni pamoja na kutumia simu za aina zote za mkononi baina ya mkulima na wataalamu kwa kutumia teknolojia hiyo ya mawasiliano itatatua changamoto nyingi.

Dkt. Emmanuel Malisa aliyekaa (kulia) na Afisa Msimamizi Mkuu wa Uhaulishaji wa Teknolojia SUA Lucy Madala wakiendelea na maandalizi ya maonesho,

Sasa tunataka kufikia hatua ya kutumia Akili Mnemba kuhakikisha kuwa mkulima yeyote ambaye ana simu yake mahali popote anaweza kupata teknolojia au taarifa iliyotokea SUA kwa wakati, tayari tumeanza tafiti kidogo kidogo na tunaamini watafiti wetu watakamilisha hilo” amesema Dkt. Malisa

Maadhimisho ya Wiki ya Elimu, Sayansi na Ubunifu yameanza leo Mei 25 na yatafunguliwa rasmi Mei 27, 2024, kauli mbiu ya maonesho hayo ni ‘Elimu, Ujuzi na Ubunifu kwa Uchumi Shindani’.

Picha chini ni watumishi na wanafunzi kutoka SUA wakiendelea na maandalizi ya maonesho










Post a Comment

0 Comments