SUAMEDIA

Wahitimu SUA wameaswa kutumia elimu na mafunzo waliyopata kuleta maendeleo nchni







Na: Siwema Malibiche,

Wahitimu  wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha kilimo (SUA) wameaswa kutumia elimu na mafunzo waliyopata  chuoni hapo  kwa  ubunifu  katika kufanya ubunifu  wa maendeleo  endelevu kwa ustawi wa taifa la Tanzania.

                                

Kauli hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa Baraza la Chuo hicho Jaji Mkuu Mstaafu Mohamed Chande Othman wakati wa hotuba yake ya utekelezaji wa majukumu ya Chuo kwenye mahafali ya 43 ya katikati ya mwaka ya Chuo hicho yaliyofanyika kwenye Kampasi ya Edward Moringe mkoani Morogoro ambapo jumla ya wanachuo 777 wamehitimu 777 masomo yao.

Amesema Baraza la Chuo limeendelea kutekeleza majukumu kwa ufanisi,  majukumu hayo ni pamoja na kuisimamia Menejimenti ya Chuo ili itekeleze majukumu makuu ya Chuo ambayo ni pamoja na kutoa mafunzo, kufanya utafiti, kutoa huduma za Kitaalamu, pamoja na shughuli za ugani.                                                                

Aidha amesema  SUA  inawatarajia wahitimu hao  wawe mabalozi wa kukitangaza Chuo vizuri kwa tabia na utendaji wao mzuri wa kazi lakini pia ni mategemeo ya Chuo kwamba watatumia elimu waliyopata kwa kufanya kazi kwa bidii, weledi na ubunifu  kwa maendeleo ya nchi.

"Mnapoingia  kwenye ulimwengu wa ajira iwe ya kuajiriwa au ya kujiajiri kumbukeni kuwa nyinyi ni mabalozi wetu katika kutunza maadili , ubunifu, na uchapakazi, maarifa na ujuzi mlioupata hapa ziwe dhana za kuleta  mabadiliko  chanya kushughulika  na matatizo ya nchi na za kidunia na kuboresha maisha  ya watanzania  na jamii kwa ujumla," ameeleza Jaji  uyo Mstaafu.

Vile vile Jaji huyo amewataka wahitimu kuyaishi maneno ya hayati Nelson Mandela ambayo yanasema  elimu ndiyo silaha yenye  nguvu zaidi  ambayo inaweza  kutumia nguvu nyingi zaidi katika kubadilisha  ulimwengu  na  anaamini kuwa  wahitimu hao wana uwezo wa kuubadilisha  ulimwengu.

 Kwa upande wake Goodluck Saltiel Maoy  muhitimu wa Shahada ya Uhifadhi wa Wanyama Pori SUA  ameipongeza Menejimenti ya Chuo kwa kuandaa  sherehe za mahafali huku akiwataka wahitimu wenzake kuyaishi  kwa vitendo yale yote ambayo wamejifunza  katika kipindi chote cha masomo chuoni hapo huku akikisisitiza kuwa yeye ataenda kuongeza elimu kwa jamii  kuhusu namna nzuri  ya kuhifadhi wanyamapori ili kukuza utalii nchini.

                                 

Naye Nicodemo Charles  Mahega muhitimu wa Shahada ya Sayansi ya Chakula na Teknolojia  amesema  anaenda kuisaidia jamii huku  akiweka wazi kuwa anatambua uwepo wa changamoto  hasa kwenye mfumo wa chakula Tanzania  na  kutokana na elimu  aliyoipata  italeta chachu   kwenda kuibadilisha jamii juu  ya matumizi mazuri ya lishe  na  kutoa wito kwa  jamii  kushirikiana  na wataalam wa lishe  ili kuhakikisha uwepo wa lishe  bora kwa watanzania wote.


Post a Comment

0 Comments