SUAMEDIA

SUA yatoa kipaumbele kwa Waandishi Waendesha Ofisi kupata Mafunzo TAPSEA

 

Na: Tatyana Celestine, Mwanza.

Waandishi Waendesha Ofisi Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) wametoa shukrani zao kwa Menejimenti ya SUA kwa kuona umuhimu wa kuwapa nafasi ya kujifunza na kukumbushwa maadili ya kazi yao kwani wanayo nafasi ya kujenga au kubomoa taswira ya Taasisi kutokana na Tabia au Utendaji kazi wawapo ofisini.

                          

Wakizungumza na SUA MEDIA wakati wa Mkutano wa 11 TAPSEA jijini Mwanza leo Tarehe 21/05/2024 wamesema kuwa Chuo kimekuwa kikiwajali na kuwapa kipaumbele katika kila nyanja na zaidi katika kuboresha utendaji kazi wao kwa kujifunza mambo mapya pamoja na kukutana na wengine kila mwaka kwenye Mkutano wa TAPSEA.

Akielezea namna mafunzo hayo yanavyoweza kuboresha taswira ya Chuo Bi.
Ritha Mashambo ambaye ni Katibu Mahsusi kutoka Kurugenzi ya Mipango na Uwekezaji- SUA amesema kuwa katika mkutano huo wanajifunza mambo mengi lakini kubwa zaidi ni utunzaji wa siri za ofisi kwa nafasi hiyo wao ndio hushika nyaraka mbalimbali kila siku hivyo pasi kukumbushwa umuhimu huo mara kwa mara ni rahisi kuweza kwenda kinyume na maadili ya kazi.

                              

Mwandishi Muendesha Ofisi huyo ameongeza kuwa wao ni kioo cha ofisi ama Taasisi kwakuwa wanatengeneza picha halisi kwa namna wanavyotoa huduma kwa kuonekana Taasisi ni nzuri au mbaya mara nyingi chanzo kinaanzia kwao, hivyo wanapongeza  menejiment kwa kutoa nafasi na  kuona umuhimu wake lakini pia amenashauri menejimenti kuendelea  kutenga fedha kwa kufanya wote waweze kushiriki kila mwaka.

Kwa upande wake Bi. Romana Kibua ambaye ni Mwandishi Muendesha Ofisi kutoka Ndaki ya Kilimo SUA amesema mafunzo hayo ni muhimu kwakuzingatia kuna waandishi waendesha ofisi wapya wanakuwepo kila mwaka hivyo ameomba Mradi wa HEET usiache kuwashika mkono katika matukio muhimu kama hayo ambayo yanajitokeza mara moja kwa mwaka ili kuendelea kuwa bora katika kazi.



Katika kuhakikisha mafunzo hayo yanaenda kama ilivyotakiwa menejimenti ya chuo imeteua muongozaji wa msafara huo nae alipotakiwa kuzungumzia hali halisi na sababu za  yeye kuwepo tofauti na miaka mingine Afisa Tawala Bi. Eliza Mtambo amaesema kuwa Menejiment imetambua umuhimu wa mkutano huo na kumtuma yeye ahakikishe kila mmoja aweze kushiriki kikamilifu katika mafunzo hayo kwani hata wawapo Mwanza haimaanishi hawapo kazini lazima wazingatie uadilifu, heshima, uchapakazi na maadili ya utumishi.

Aidha Bi. Mtambo amewataka viongozi wanaoandaa Mkutano wa TAPSEA kuanza kufanya maadhalizi mapema hasa katika usajili ambapo kwa mwaka huu wanatumia teknolojia mpya ya usajili (Control Number)  ili kuondoa sintofahamu kwa wale ambao wamelipia na wamefika hawaruhusiwi kuinguia moja kwa moja badala yake wanakaa nje kwa muda mrefu kutokana hilo inapelekea washiriki kushindwa kupata kile walichotarajia kwa kukosa kujifunza mada muhimu.      


   








  
     

Post a Comment

0 Comments