SUAMEDIA

SUA kupongezwa kupeleka Waandishi Waendesha Ofisi kutoka Kampasi ya Olmotonyi TAPSEA -Mwanza

Na: Tatyana Celestine

Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kimepongezwa kuzingatia kutoa fursa kwa Waandishi Waendesha Ofisi wageni waliohamia, waliobadilisha Kada na kwa mara ya kwanza kutoka Kampasi ya Olmotonyi wameweza kushiriki katika kujifunza mafunzo mbalimbali ambayo yatawasaidia katika majukumu yao ya kila siku kazini hata kwenye familia zao.

                            

Akizungumza na SUAMEDIA Mwenyekiti wa Waandishi Waendesha Ofisi SUA Bi. Joyce Mwiyola amesema kwa miaka miwili sasa kumekuwa na mabadiliko ya madhurio katika Mkutano huo kwa upande wa SUA kwani wamekuwa hawashiriki wote hivyo ameomba menejimenti ya SUA kujitahidi kuhakikisha wanashiriki wote kwani mafunzo hayo hayajirudii na ni ya muhimu kwao.

                     

Kwa upande wake Mwandishi Mwendesha Ofisi kutoka Kampasi ya Olmotonyi SUA- Arusha Bi.  Abia John amesema anaishukuru Menejimenti ya SUA kwa kuwakumbuka mwaka huu kushiriki kwa mara ya kwanza binafsi amejifunza mengi aliyokuwa hayajui ambayo yanamfanya aende kutenda kazi zake kwa weledi na ubora.

Aidha ameomba kutoishia hapo wazidi kuwafikiria hata wale ambao wapo katika kampasi nyingine kushiriki kwa miaka ijayo kutokana wanapokosa mafunzo hayo hawatapata tena na hii ni kutokana na TAPSEA kuhakikisha wanagusa kila eneo ikiwemo Afya ya akili, Maadili katika kazi, utunzaji wa siri za ofisi kubadilika kila mwaka.

Kwa kujibu changamoto iliyowasilishwa na muongoza msafara kutoka SUA Afisa Tawala Bi. Elizabeth Mtambo ya kuwataka viongozi wanaoandaa Mkutano wa TAPSEA kuanza kufanya maadhalizi mapema, SUA MEDIA imetaka ufafanuzi kutoka kwa Mwenyekiti wa Waandishi Waendesha Ofisi TAPSEA Morogoro Bi Hellen Magati amesema changamoto imekuwepo kutokana na upya Teknolojia ya kufanya usajili hivyo amewataka wanachama wote kuhakikisha wanajisajili kupitia online ili kuondokana na adha kama iliyojitokeza kipindi hiki.

Bi. Magati ameongeza kuwa ili kuweza kutatua changamoto ya wanachama kukosa mafunzo wanachama wote wameruhusiwa kuingia kujifunza wakati wanaendelea kujisajili sambamba na hilo amewataka wanachama kuhakikisha wanalipia mapema kwani mwanzo  wale ambao hawakulipa kwa wakati walilazimika kubaki nje kupelekea kupitwa na mafunzo.


















Post a Comment

0 Comments