SUAMEDIA

SUA toeni elimu mliyoipata ya tahadhari na kukabiliana na majanga - Mkaguzi wa Jeshi la Zimamoto Veronica John

 Na: Siwema Malibiche

Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoani Morogoro limewataka wafanyakazi katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo ambao wameshiriki mafunzo ya kukabiliana na majanga mbalimbali kuwa mabalozi wazuri na kuielimisha  jamii namna ya kukabiliana na hali hiyo inapojitokeza.

Wafanyakazi SUA wakishiriki katika zoezi  la majaribio ya kuzima moto katika Kampasi ya Edward Moringe Sokoine 

Akizungumza katika mafunzo ya siku mbili yanayofanyika katika Kampasi ya Edward Moringe Sokoine kuazia Mei 20, 2024 Mkaguzi wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoa wa Morogoro Veronica John amesema Jeshi hilo linapofanyakazi ya uoakoaji hakuna gharama yoyote inayotozwa kwani huduma zote zinatolewa bure.

Amesema ni vyema washiriki kuzingatia kwa makini mambo yote watakayojifunza hasa tahadhari  katika makazi na namba bora ya kukabiliana na majanga yakiwemo ya moto ambayo hugharimu Maisha na mali za watu.

Mkaguzi wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoa wa Morogoro Veronica John akiongea na wafanyakazi wa SUA, hawapo pichani (Picha na zote na Ayoub Mwigune)

Aidha amewataka wananchi kuachana na ujenzi holela ambao unasababisha kuchelewa kwa waokoaji kufika katika eneo lilitokea janga na badala yake jamii ishirikiane na Jeshi hilo katika usomaji wa ramani ili kuwa na mpangilio mzuri wa majengo utakaowezesha uwepo wa miundombinu rafiki.

Kwa upande wake Jumanne Yusuph,  Mrakibu Msaidizi wa Polisi Wasaidizi  SUA amelipongeza Jeshi la Zimamoto na uokoaji kwa kutoa  mafunzo ya kinga na tahadhari   kwa wafanyakazi SUA  na ametoa wito kwa wafanyakazi wote waliopata mafunzo hayo waende kutoa elimu kwenye  jamii kuanzia ngazi ya familia na hasa kwa watoto ili kusaidia kuongeza tahadhari, kupunguza  na  kuepusha madhara  yanayoweza kujitokeza. 

Nae Lucas Iyera  mshiriki   katika mafunzo hayo ameupongeza uongozi wa Chuo kwa kushirikana na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kuandaa mafunzo hayo  ambayo yanasaida kuwakumbusha  namna  mwananchi anaweza kuchukua tahadhari katika kujikinga  na majanga mbalimbali.

Picha chini ni watu ni matukio mbalimbali katika mafunzo hayo











Post a Comment

0 Comments