SUAMEDIA

Waandishi Waendesha Ofisi wanatakiwa kutambua kukaa muda mrefu ni hatari kuliko ulaji mbaya

Na: Tatyana Celestine

Waandishi Waendesha Ofisi wametakiwa kutambua asilimia 80 katika utendaji wao ni kuhakikisha wanaweka mambo yaende sawa katika ofisi lakini wasiache kuzingatia afya wawapo mahala pa kazi kwani sayansi inasema  kukaa muda mrefu ni hatari zaidi  kuliko ulaji mbaya ambao upelekea vifo vingi.

                              

Katika Mkutano wa 11 TAPSEA jijini Mwanza Mwezeshaji ambaye pia ni Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Figo Garvin Kweka kutoka Hospitali ya Rufaa ya Muhimbili jinini Dar es salaam akizungumzia Afya ya akili amesema kuwa  Waandishi Waendesha Ofisi wanatakiwa watambue maisha yanahitaji Afya ya mwili, Hisia, dini kwa kuwa vitu vyote hivi vitapelekea mwanadamu kuwa na maisha marefu na kuwaepushia magonjwa yasiyo ya lazima lakini pia kuyakabili.

                              

Daktari huyo ameweka bayana kwamba matendo ya mwanadamu anayoyafanya katika umri alionao ndio yanapelea kuishi kwa afya bora au la hapo baadae kwani wagonjwa wengi magojwa yao huchangiwa na tabia hatarishi kama vile ulevi, ulaji mbaya na zinaa ambazo ndio zinakusanya magonjwa yote yanayotesa watu kwa sasa.

                               

Aidha amesema wafanyakazi wengi wanaangalia zaidi namna ya upatikanaji wa pesa na mali na kusahau afya zao bila kujua mwanadamu anapofika umri kuanzia miaka 40 ndio anatakiwa kuzingatia afya zaidi kuliko utafutaji wa mali na fedha maana hata akizipata hawawezi kuzitumia vizuri ikiwa afya yake sio nzuri matokeo yake gharama kubwa za matibabu hutumika kwa kutibu maradhi ambayo yangeweza kuzuilika hapo kabla.

                               

 Pia Dkt. Kweka ameeleza kuwa Waandishi Waendesha Ofisi wasipozingatia Afya wapo katika hatari ya kupata magonjwa ya mifupa, mgongo, mumivu ya mwili, unene ulipitiliza, saratani, kisukari ambayo yatakulazimisha utumie dawa matokeo yake wanaweza kuua figo hivyo kuanzia sasa waangalie viti wanavyotumia kukaa ofisini, unywaji wa maji, kula kwa kiasi pamoja na mazoezi.

                              

Katika upande mwingine amewaasa wafanyakazi ambao wanashindwa kuzingatia malezi ya watoto wao kwa kuwapa kila kitu wanachotaka kula pasi kuzingatia chakula bora matokeo yake wanaanza kuugua magonjwa kama kisukari na moyo wakiwa wadogo huku wazazi wengine kushindwa kuwalinda watoto wao kupelekea majanga kama ubakaji, ulawiti, uvutaji shisha, ulevi hatimaye wakija kugundua tatizo linakuwa limekwishakuwa kubwa hivyo wafanyakazi wasiwasahau watoto hata kama wana kazi nyingi.


                            
















Post a Comment

0 Comments