SUAMEDIA

Mafunzo ya Amali na kuasili teknolojia ni suluhisho la ajira na utatuzi wa changamoto

 Na: Gerald Lwomile

Imeelezwa kuwa utashi wa kisiasa, ukweli kuhusu kuingia kwenye mapinduzi ya nne ya viwanda na kutatua changamoto mbalimbali ni baadhi ya mambo ambayo hayakwepi na suluhisho lake ni kuwa na teknolojia bora na elimu ya amali.

Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Carolyne Nombo

Hayo yamesemwa leo Mei 28, 2024 na Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Carolyne Nombo, wakati akizungumza katika Kongamano la Elimu, Ujuzi na Ubunifu lililofanyika katika ukumbi wa Tanga Beach Resort jijini Tanga.

Prof. Nombo amesema mafunzo ya amali ambayo miaka ya nyuma yalikuwa yakifundisha tangia shule za msingi na sekondari na yalijulikama kama Sayansi Kimu kwa shule za msingi na katika shule za sekondari wanafunzi walisoma Uhandisi, Mapishi, Kilimo na masomo mengine mengi ambayo yalimuandaa kijana kuwa na ujuzi na kumuweka katika soko la ushindani kwa kupata ajira au kujiajiri.


Amesema tayari vyuo vikuu vina miongozo kuhusu aina hii ya elimu na vimeeendelea kujenga mahusiano mazuri na viwanda binafsi ili kuhakikisha mwanafunzi anapata zaidi mafunzo ya vitendo ya fani anayochukua.

Akizungumza katika kongomano hilo, Mwenyekiti Mtendaji wa AfricAcademy-Arusha Science na Mhadisi Kilimo Prof. Nuhu Hatibu amesema mifumo mingi hivi sasa inatumia teknolojia za kisasa hivyo kama taifa hakuna sababu ya kusubiri na watu hasa vijana na watoto kuonyeshwa njia ya kuasili mifumo hii.


Amesema mafunzo ya amali ni vyema yakaenda sako kwa bako na kuzipokea, kuvumbua na kuziendeleza teknolojia mbalimbali kwani dunia ilipofikia sasa kama utachelewa kidogo tu katika kuzijua na kuzitumia teknolojia basi utachwa mbalimbali na kushindwa kuzalisha kwa wingi.

Akizungumzia mifumo ya kidijiti Bi. Winfred Ng’ang’a kutoka Kampuni Tanzu ya ‘Amazon Web Services’ ya nchini Kenya ambayo hutoa huduma za kidijitali kwa kutumia mfumo wa uandaaji wa program kidijiti wao wamefanikiwa kuhakikisha wanafunzi katika nchi ya Kenya wanakuwa na jukwaa ambalo linawasaidia kupata taarifa mbalimbali na pia wanaweza kuwa taarifa zao.

Bi. Winfred Ng’ang’a kutoka Kampuni Tanzu ya ‘Amazon Web Services’ ya nchini Kenya akielezea uzoefu wa Kampuni yao ya AWS 



Post a Comment

0 Comments