SUAMEDIA

Wanataaluma SUA waaswa kuwatambua Watu wenye Mahitaji Maalumu ili kuondoa tabia kandamizi

      

Na, Tatyana Celestine, Winifrida Nicholaus

Watu wenye mahitaji maalumu wanatakiwa kujumuika katika jamii ili nao waweze kukabiliana na hali zote kama serikali ilivyotaka shule zote zihusishe wanafunzi wa aina mbalimbali bila kujali hali zao kwa kuwataka kuendana na halisi pindi watakapomaliza masomo yao waweze kufanya kazi na watu wa aina zote pasi ubaguzi.

                    

Akizungumza na wanataaluma katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) Mhadhiri kutoka  Chuo Kikuu cha Dar-es - Salaam Dr. Lwimiko Sanga katika kuwajengea uwezo juu ya watu wenye mahitaji maalumu na kusema kuwa Shule zote na Vyuo vinatakiwa kuzingatia miundombinu stahiki kwa wote kwani wakati umefika Serikali kupitia Mradi wa Elimu ya Juu kwa Mabadiliko ya Kiuchumi (HEET)  imeamua wanafunzi wote waweze kupata elimu kwa usawa.

Dkt. huyo amebainsha kuwa mifumo ya Elimu aina mbili nchini imeleta changamoto kubwa kwa watu wenye mahitaji maalumu kushindwa kufanya vema katika masomo na pia kushindwa kuchanganyika katika jamii ambapo kupelekea utofauti katika kila hatua zao za kutafuta elimu kwani kuna watu wa aina tofauti kama vile wasiiona, watu wenye ulemavu wa macho, watu wenye ulemavu wa viungo na wengine ulemavu unawajia baadae katika miangaiko ya maisha.

Aidha ametaja mifumo hiyo ya kielimu kama vile mfumo wa elimu maalum na mfumo rasmi ambapo hugawa wanafunzi kulingana na mifumo hiyo kitu ambacho kinapelea jamii kutengeneza  namna isiyofaa ya kuwatambua kwa majina  ikiwemo kilema, kiwete, kipofu, Zeruzeru na wasiosikia kwa ujumla majina hayo ni kandamizi.

Amesema mafunzo hayo yaliyotolewa kwa wanataaluma yawe chachu katika kuzingatia kuwatambua, kuwasaidia kufikia malengo, kuwajali, pia kutafuta ufumbuzi wa changamoto katika upatikanaji wa elimu kwa wanafunzi wao pamoja na kutengeneza usawa kwenye Vyuo, Jamii na Taifa kwa ujumla.

“Jamii nyingine imekuwa ikiua Watoto walemavu kwa kuona ni laana ama mkosi….sisi wote ni binadamu hatutakiwi kuonesha unyanyapaa kwani sote ni walemavu kwa namna tofauti, kama tutapimwa kila mmoja atatambua lakini pia wengine ulemavu huja kwa ajali, umri, kurithi na mengineyo” amesema Dr. Sanga.






 


Post a Comment

0 Comments