Na George
Balozi wa Norway Nchini
Tanzania Mhe. Tone Tinnes amesema nchi ya Norway itaendeleza ushirikiano na Chuo
Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA), ambao umedumu kwa zaidi ya miaka 50 hadi
hivi sasa.
Balozi Tinnes amesema
hayo Aprili 22, 2024 ambapo pamoja na
mambo mengine amefanya mazungumzo na Makamu Mkuu wa Chuo hicho Prof Raphael
Chibunda pamoja na Marasi wa Ndaki, Wakurugenzi na Watumishi wa Idara
mbalimbali chuoni hapo.
Mhe, Balozi Tone amekiri
kufurahishwa na kile kinachofanyika SUA
ikiwemo kuelimisha watu hususani wakati huu wa Mabadiliko ya Tabia ya Nchi, kufundisha watu juu ya kilimo
bora na cha kisasa hususani Kilimo Biashara.
Kwa upande wake Makamu Mkuu
wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo Prof. Raphael Chibunda amesema kuwa ziara
hiyo ya Mhe. Balozi Tone ni matokeo ya Mkataba wa Makubaliano uliosainiwa baina
ya SUA na Chuo Kikuu cha Sayansi ya Maisha cha Norway ‘Norwegian University
of Life Sciences’ ambapo makubaliano hayo yamelenga katika Sekta ya Kilimo
ili kuwawezesha wakulima kukabiliana na Mabadiliko ya Tabia ya Nchi lakini pia
kuweza kufanya tafiti mbalimbali.
Prof. Chibunda amesema
makubaliano hayo yamelenga pia katika kubadilishana uzoefu kati ya Vyuo hivyo ikiwemo wataalam mbalimbali wa Vyuo Vikuu, Walimu,
Wanafunzi pamoja na Watafiti.
Katika ziara hiyo Balozi
Tone ametembelea miradi mbalimbali iliyopo chuoni hapo iliyofadhiliwa na Nchi
ya Norway, ikiwemo Kituo cha Taifa cha Kuratibu Hewa Ukaa , Kituo cha Kujifunzia Kilimo Atamizi
cha Kilimo Biashara, Maabara ya Sayansi iliyopo Kampasi ya Solmon Mahlangu, pia
ametembelea Shamba la Mafunzo la Viumbe Maji na kujionea namna ya ufugaji na
utunzaji wa Samaki aina ya Sato na Kambale.
Itakumbukwa kuwa mwezi Februari, 2024 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan alipokuwa ziarani nchini Norway alisaini mikataba mbalimbali ikiwemo Mkataba wa Kuimarisha Sekta ya Kilimo, pamoja na Hati ya Makubaliano ya Ushirikiano wa Chuo Kikuu cha SUA uliosainiwa na Makamu Mkuu wa Chuo Prof. Raphael Chibunda
0 Comments