SUAMEDIA

Wafanyakazi wametakiwa kuzingatia kupima Afya , ulaji unaofaa

 

Na: Tatyana Celestine, Winfrida Nicolaus      

Wafanyakazi wametakiwa kuzingatia kupima Afya pamoja na ulaji unaofaa kwani ni jambo la muhimu kwakuwa mfanyakazi mwenye afya bora ni  mtaji katika uzalishaji ambapo mwajili ananufaika kupitia yeye kwaweza kutekeleza majukumu yake kikamilifu na ufanisi kufikia malengo ya Taasisi hata Taifa mahala pa kazi.



Kauli hiyo imetolewa na Dkt. Erhard Kapilima kutoka Kurugenzi ya Huduma za Afya Hospitali ya Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo SUA wakati akizungumza  kwenye Mkutano Mkuu wa Chama cha Wafanyakazi wa Taasisi za Elimu ya Juu Tanzania (THTU) Tawi la SUA ambapo amesema elimu ya masomo yahusuyo Afya ni muhimu kwa wafanyakazi kwakuwa watatambua aina za magonjwa vilevile visababishi vya magonjwa hayo hasa yale magonjwa sugu yasiyoambukizwa ambayo mara nyingi yanatokana na mitindo ya maisha.

“La msingi magonjwa haya sugu yasiyoambukizwa yameongezeka kwa kiasi kikubwa na kusababisha nguvu kubwa ya utendaji kazi kupotea hivyo nitoe wito kuzingatia nidhamu ya ulaji kwa kuwa ndio tatizo kubwa vilevile utaratibu wa kufanya mazoezi na matumizi ya sigara pamoja na pombe kupita kiasi ni kati ya vitu vikubwa vinavyozorotesha afya na kuharibu kabisa utendaji kazi”, amesema Dkt. Kapilima

Dkt. Kapilima ameongeza kwa kusisitiza Chama cha Wafanyakazi THTU kimeatoa elimu ya afya kwa wanachama wake hivyo isiishie hapo yanapaswa  kuwa endelevu kwakuwa ni chachu ya kufungua watu uelewa wao ili kuweza kuchukua hatua stahiki katika kuhakikisha afya zao zinakuwa imara katika kurahisisha utendaji kazi,

Amesema wafanykazi wanapotambua masuala hayo inawasaidia kuchukua hatua kujikinga na kuboresha afya zao zaidi kwenye mazingira ambayo wanafanyia kazi. na kwa yule ambaye anahisi anahitaji kujua zaidi Hospitali yao ya SUA inatoa huduma ya kuelimishs vilevile  bado  chuo kupitia hospitali inafadhiri vipindi vya redio kupitia SUA FM kuhusu masuala ya afya.

Kwa upande wake Dkt. Prisila Mkenda Mhadhiri SUA kutoka Idara ya Sayansi ya Viumbe Hai ambaye pia ni mwanachama wa THTU amesema wamekuwa na wakati mzuri kutokana na mafunzo waliopatiwa yamekuwa ni ya msingi  kwao hasa kwa upande wa afya kuhusiana na namna gani wanaweza kujikinga na magonjwa sugu yasiyo ya kuambukizwa ambayo yamekuwa ni tatizo sana kwenye jamii hivyo  kwa elimu hiyo itasaidia  kubadili namna wanavyoishi.                                              

“Tumekuwa tukila vyakula ambavyo ni vya kisasa zaidi na kusahau vile vyakula vyetu vya asili ambavyo pengine vina afya na manufaa mwilini kuliko hivi vya kisasa vilevile tumekuwa ni watu ambao hatuna mazoezi Wala kutembea umbali wowote mara nyingi tumekuwa tukitumia magari, kukaa ofisini, kula na kulala hivyo mafunzo haya yametupa namna ya kutafakari na kubadili mienendo yetu ya maisha ili kulinda afya zetu na kudanya kazi kwa uadilifu kwasababu afya zetu ni imara”, amesema Dkt. Prisila Mkenda

 












Post a Comment

0 Comments