Na: Tatyana Celestine
Wafanyakazi wote wametakiwa kutambua kuwa nafasi ya mfanyakazi bora ni sehemu ya kuchaguliwa na sio jambo ambalo mtu amezaliwa kwamba lazima apate na endapo hatopata haina maana ya kukosa sifa zaidi ni kuzingatia kuendelea kufanya kazi kwa bidii na ufanisi katika maeneo yao ya kazi pasi kujenga chuki na mitafaruku.
Akizungumza na wafanyakazi bora wanataaluma na waendeshaji waliochaguliwa katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kwenye kikao cha uchaguzi wa kumpata Mfanyakazi Bora wa Chuo atakayewakilisha Chuo kimkoa, Naibu Makamu wa Mkuu wa Chuo Mipango, Fedha na Utawala Prof. Amandus Muhairwa amesema kuwa yeye binafsi hajawai kuwa mafanyakazi bora tangu alipoanza kazi kwa atakribani miaka 31 na wala haoni kama hiyo inamuondolea sifa ya kuendelea kufanya kazi kwa bidii.
"Kuna watu wanapata jazba wanapokosa nafasi ya Mfanyakazi Bora na kuamua kuchukia pamoja na kusababisha matatizo kama kutoa malalamiko, mtu wa namana hii anaitwa king'ang'anizi na inawezekana akawa anamatatizo kisaikolojia... nafikiri mfanyakazii unatakiwa kufanya kazi kwa weledi pasi kulalamika" amesema Prof. Muhairwa.
Wakati
huohuo wafanyakazi bora 36 wakiwemo wanataaluma na waendeshaji SUA wameshiriki
kumchagua mfanyakazi bora wa Chuo namba moja na namba mbili ambao
watakiwakilisha chuo kimkoa.
Kwa
upande wake Mshindi wa Kwanza katika uchaguzi huo Bw. Kundansen Swai amesema
kuwa ushindi wake umetokana kukisaidia Chuo katika kuhakikisha kila mfanyakazi
anawasilisha taarifa zake katika mfumo mpya wa PEPMIS ambao ametumia muda wake
hata usiku ili kila mmoja kufanikisha kujaza taarifa zake kikamilifu na kuwataka
wafanyakazi wote kujituma na kuwahi kazini, kuipenda kazi anayoifanya pamoja na
kuwa muwajibikaji bila kujali malipo.
Naye Dkt. Alcardo Barakabize ambaye ni Mhadhiri kutoka Ndaki Asilia na Tumizi SUA akizungumza baada ya uchaguzi huo kutokana na kuibuka mshindi wa pili katika kuwakilisha Chuo amesema kutokana na kujituma, ubunifu katika kazi, uandishi wa machapisho pamoja na ushiriki katika miradi mbalimbali ndio imempa sifa kushika nafasi hiyo na kuahidi kuendelea kufanya kazi kwa bidii kwa manufaa ya Chuo yeye binafsi na taifa kwa ujumla.
Maadhimisho ya Mei Mosi mkoani Morogoro yatafanyika Ifakara lakini kwa Chuo yatafanyika
katika Kampasi Kuu ya Edwwrd Moringe kwa
Katika picha
0 Comments