SUAMEDIA

SUA kukuza ubora wa huduma na uzalishaji bidhaa

 Na: Siwema Malibiche

Wafanyakazi katika vitengo vya uzalishaji Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA),  wametakiwa kuzingatia mafunzo waliyopata ili  kukuza ubora wa huduma na  bidhaa zinazotolewa  SUA.

Rasi wa ndaki ya Uchumi na Stadi za Biashara kutoka SUA Dkt. Damas Philip akifunga mafunzo ya vitengo vya uzalishaji SUA (Picha zote na Ayoub Mwigune)


Hayo yamesemwa na Rasi wa ndaki ya Uchumi na Stadi za Biashara kutoka SUA Dkt. Damas Philip alipokuwa akizungumza na washiriki wa mafunzo hayo kutoka vitengo zaidi ya 45 vya uzalishaji  walioshiki mafunzo ya siku mbili katika  Kampasi ya Edward Moringe mkoani Morogoro  .

Amesema SUA ni miongoni mwa Taasisi za Serikali zenye rasilimali   nyingi ambazo zinatakiwa kutumiwa  kwa usahihi ili kuleta tija  chuoni na taifa kwa ujumla  kwa kuongeza uzalishaji katika vitengo  vilivyopo   ili kuongeza ufanisi katika uzalishaji. 

Nimefurahi kusikia kuwa wawezeshaji ambao wametumika katika mafunzo haya wametoka ndani ya chuo ambao wanakifahamu chuo vizuri  na fursa zilizopo na hii imeonyesha namna nzuri ya kutumia rasilimali tulizonazo kwa kuleta maendeleeo kwa taasisi na nina amini mafunzo haya  ya siku mbili hayajapotea bure na kila kitu kitatiliwa maanani  ”, amesema Dkt. Philip.

Naye, Suma  Mwakanenela  kutoka Ndaki ya Uchumi na Stadi za Biashara  ambae alikuwa muwezeshaji wa mafunzo hayo, amesema  kuwa mafunzo hayo yatasaida  kukuza uzalishaji katika vitengo mbalimbali ndani ya SUA,   iwapo  yatafanyiwa kazi  kwa kuongeza ubora kwa kutumia  ubunifu na fursa ipasavyo  ili kuongeza uzalishaji.

Suma  Mwakanenela  kutoka Ndaki ya Uchumi na Stadi za Biashara  ambae alikuwa muwezeshaji akifafanua namna mafunzo hayo yatakavyosaidia katika uzalishaji SUA


Kwa upande wake mmoja wa washiriki katika mafunzo hayo Bakari Mohamed Abdallah kutoka  Shule Kuu ya Uhandisi na Teknolojia SOET   amewashukuru, waandaaji wa mafunzo hayo kwa kuwaongezea uelewa    wa  namna nzuri ya kutumia fursa  na amekiri kujua vitu vingi ambavyo awali hakuwa akivijua mfano matumuizi ya busara katika utoaji huduma kwa wateja.

Naye Grace Kajuna Afisa Utumishi kutoka Taasisi ya Elimu ya  Kujiendeleza, ICE  SUA amesema mafunzo hayo yamemuongezea uelewa  hasa namna mzuri ya kutumia fursa zilizopo kwenye  kuongeza pato  la Chuo na  anatatarajia kuboresha huduma anazozifanya  katika kitengo chake na ameahidi kuyatekeleza yote aliyojifunza katika uzalishaji.

Picha chini ni wafanyakazi katika vitengo vya uzalishaji SUA 👇







Post a Comment

0 Comments