Na:Winfrida Nicolaus, Tatyana Celestine
Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kimeendelea kuhakikisha elimu inayotolewa chuoni hapo kuendana na soko la ajira kwa kupitia mitaala na kufanya mabadiliko katika ufundishaji kwa lengo la kuifanya Sekta ya Kilimo kutazamwa kibiashara.
Akifungua Mafunzo kwa Wanataaluma wa SUA pamoja na washiriki kutoka Mtandao wa Vyuo Vikuu
vya Kilimo katika nchi za Afrika (RUFORUM) kwa niaba ya Makamu Mkuu wa Chuo
hicho Prof. Raphael Chibunda, Rasi wa Ndaki ya Uchumi na Stadi za Biashara
kutoka SUA Dkt. Damas Philip amesema warsha hiyo inamchango mkubwa hasa katika
zoezi la kupitia na kuanzisha Mitaala mipya ya Shahada za ngazi tofauti.
Kwa
upande wake Rasi wa Ndaki ya Kilimo SUA Dkt. Nyambilila Amuri amesema SUA inatoa
mafunzo kwenye programu mbalimbali za kilimo na kitu pekee wanacholenga kukipata katika Mafunzo hayo ni kukifanya
kilimo kuwa chanzo cha ajira inayoleta tija lakini pia kutatua changamoto ya
ajira kwa vijana nao kuweza kushiriki kikamilifu
katika kilimo.
Dkt.
Amuri Amesema kutokana na mageuzi makubwa ya kiteknolojia na uchumi ndani na
nje ya nchi, SUA kama Vyuo Vikuu vingine
vyote Duniani kimelazimika kufanya mabadiliko katika mitaala inayolenga zaidi
kuwapa wanafunzi fursa ya kujifunza na kugundua lakini pia kufanya kwa vitendo
ili waweze kuelewa zaidi na kwenda kukiboresha kilimo.
“Katika
warsha hii tunaendelea kuboresha pale tulipofikia lakini pia kupaboresha zaidi
ili tuweze kumtoa muhitimu yule ambaye ataleta maendeleo, uelewa mkubwa,
nidhamu, ufanisi lakini pia wale ambao wanaweza kuwasiliana na kitu alichokijua kwa hali yoyote”, amesema
Dkt. Nyambilila Amuri.
Kwa upande
wake Dkt. Florence Nakayiwa Naibu Katibu Mtendaji wa RUFORUM amesema RUFORUM ni
Mtandao wa Vyuo Vikuu 170 kutoka nchi 40 za Afrika na SUA ikiwa miongoni mwao
kwa lengo la kushirikiana ili kuhakikisha wanafanya kazi kwa pamoja
katika kuboresha Mitaala itakayoleta umuhimu kwa wakulima, wanafunzi, watu
katika jamii na kukifanya chuo kikuu kuangalia
kama mwezeshaji wa maendeleo.
0 Comments