SUAMEDIA

Wanataaluma SUA kuwatambua wanafunzi wenye mahitaji maalumu katika kutengeneza usawa

 Na: Tatyana Celestine, Winfrida Nicolaus

Wanataaluma Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) wametakiwa kuwatambua wanafunzi wenye mahitaji maalumu katika kutengeneza usawa kwa kutoa elimu stahiki kwani Serikali ya Tanzania kupitia Mradi wa Elimu ya Juu kwa Mabadiliko ya Kiuchumi (HEET) imewezesha Vyuo vikuu kuhakikisha vinamjali na kumpatia elimu mwanafunzi mwenye mahitaji maalum kama wanafunzi wengine.

                             

Katika kuhakikisha hilo linatekelezeka kikamilifu kwa kumuunga mkono Rais Samia Suluhu Hassan Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kimeendelea kutoa elimu katika kuwajengea uwezo wanataaluma ili  kuwatambua na kuwahudumia wanafunzi wenye mahitaji maalum kulingana na mahitaji yao pamoja na kuwawezesha kutimiza malengo.

Amebainisha hayo Mratibu wa Kitengo cha Elimu Jumuishi na Mahitaji Maalum chini ya Mradi wa Elimu ya Juu kwa Mabadiliko ya Kiuchumi (HEET) ambaye pia ni Mhadhiri Mwandamizi na Mkuu wa Idala ya Mitaala na Ufundishaji Dkt. Thabita Lupeja na kusema kuwa wanataaluma wanatakiwa kufahamu kwamba wao ni watatuzi wa changamoto ambazo wanafunzi wanakumbana nazo na ni muhimu kupata suluhisho la changamoto hizo.

Kwa upande wake Kaimu Amidi wa Shule Kuu ya Elimu SUA Dkt. Jamal Jumanne amesema jamii jumuishi kama SUA kuna watu wenye mahitaji maalum hivyo elimu iliyoandaliwa kwa wanataaluma itakuwa ni chachu katika kusaidia usawa unapatikana kwa kila mwanafunzi bila kujali jinsi, umri, pia uwezo hivyo kitu pekee kinachohitajika ni huduma bora yenye uwezo wa kumfika kwa wakati na urahisi.

                                 


Naye Mkuu wa Idara ya Misingi ya Elimu na Ufundishaji ambaye pia ni Mhadhiri wa SUA Dkt. Imelda Gelvas amesema SUA kuna wanafunzi wenye mahitaji maalum hivyo mafunzo hayo yamewawezesha kujifunza ni jinsi gani wataweza kuwajumuisha wanafunzi wote katika suala la kujifunza, kufahamu majina stahiki kwa wale wote wenye mahitaji maalum pamoja na nyenzo sahihi katika mazingira ya ufundishaji ili waweze kufikia malengo.

                                 

“Mafunzo haya yamekuwa na mchango mkubwa sana katika kutuongezea uwezo juu ya namna ya kutoa huduma kwa wanafunzi wetu wenye mahitaji Maalum hivyo niiombe Menejimenti iwasaidie pia wanafunzi lakini pia wafanyakazi wengine kupata elimu kama hii ili kurahisisha utendaji wa kazi katika kufikia lengo la kila mmoja mmoja lakini pia Taasisi”, amesema Dkt. Imelda Gelvas.

 

KATIKA PICHA 














KWA PICHA ZAIDI COPY  LINK HAPA CHINI

https://tatyana35.pixieset.com/workshoponcapacitybuildingtoacademicstaffandtechnicialstaffonspecialneedsandinclusiveeducation/

Post a Comment

0 Comments