SUAMEDIA

Mitaala yenye kuzingatia uwezo kumuwezesha muhitimu wa Chuo kuwa tayari katika Soko la Ajira

 

Na: Tatyana Celestine, Winfrida Nicolaus

Imeelezwa kuwa ni vyema kutengeneza Mitaala yenye kuzingatia uwezo ili kumuwezesha muhitimu wa Chuo Kikuu kuhitimu akiwa tayari kwenda kufanya kazi kulingana na vigezo vya mahitaji ya soko la ajira na sio kuwa na shaada pekee.                          


Amebainisha hayo Mtaalam wa Mitaala kutoka nchini Uganda Dkt. Gillian Kasirye wakati akizungumza na SUAMEDIA kwenye Mafunzo yaliyowakutanisha Wataalamu kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo pamoja na wajumbe kutoka  Mtandao wa Vyuo Vikuu vya Kilimo katika nchi za Afrika (RUFORUM) ambapo amesema walimu wengi wanalijua somo lakini hawajui jinsi ya kubuni kwa namna  ambayo litawashawishi wanafunzi kuelewa.

Amesema kila chuo kina kitivo  na kozi tofauti ni kawaida kubeba taarifa nyingi ikiwemo za kinadharia, lakini pia maudhui mengi hivyo wanapoongelea kuhusu uwezo kujumuishwa katika Mafunzo ikiwemo kuzingatiwa kwa wanafunzi, kufundishwa kupokea ujuzi, maarifa na mitazamo ili wanapohitimu wakakidhi vigezo katika soko la ajira.

“Dunia kwa sasa imeshakuwa Kijiji ndio maana tunasisitiza Digital Marketing kwa lengo la kuwajengea uwezo wanafunzi ili waende kukidhi vigezo sokoni ndio maana ukitoa mafunzo kwa wanafunzi wako wataweza kufungua mitandao yao ya kijamii vilevile kuanza kujitangaza hata kabla hawajahitimu na hilo ndio swala la muhimu zaidi”, amesema Dkt. Gillian Kasirye.

Dkt. Kasirye ameongeza kuwa SUA tayari kimeanza kupitia na kutengeneza Mitaala yao hivyo kupitia Mradi wa RUFORUM umewezesha kufanya kazi pamoja nao ili kuongeza nguvu kwa kile ambacho wamekwishafanya kwa kupita mitaala nakutengeneza utendaji kazi mzuri na kutoa uhakika wa wanafunzi kuweza, kupata elimu bora, kuongeza ushawishi kwa vijana na pia kukabiliana na soko la ajira



 Kwa upande wake Mhadhiri kutoka wa Idara ya Sayansi ya Chakula na Uchakataji wa mazao kutoka SUA Dkt. Alex Wenaty amesema kilimo kina nafasi kubwa katika ulimwengu wa sasa wa Digital Marketing kwasababu mazao yanayozalishwa na kazi zinazofanyika zinategemea sana uwepo wa digital marketing tofauti na hapo zamani ambapo kila mmoja amekuwa akienda  kwa namna alivyowezeshwa kujifunza.

Aidha ameongeza kuwa katika utoaji wa mafunzo ni muhimu kuzingatia soko linahitaji nini na hiyo itawasaidia wao kama wakufunzi kuwafundisha wanafunzi wao kwa namna ya kuwafanya kuwa bidhaa ili kuendana na ulimwengu wa sasa pia watategemea sana kufanya yale waliojifunza darasani kwani watatumia uzoefu walioupata chuoni kutumia teknolojia.

“Naiomba Menejimenti yetu ya SUA iendelee kutuwezesha zaidi katika suala zima la Mafunzo  hivyo kama itawezekana tupate muda zaidi wa kujifunza ili tuweze kupata mambo mengi zaidi na kwa wakati kwaajili ya kuwafundisha wanafunzi wetu”, amesema Dkt. Wenaty




KATIKA VIDEO BOFYA HAPA CHINI



Post a Comment

0 Comments