SUAMEDIA

Hayati Edward Sokoine alijua kutunza Mazingira - Balozi Joseph Sokoine

 Na Gerald Lwomile.

Imeelezwa kuwa Hayati Edward Moringe Sokoine, aliyewahi kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa Utawala wa Awamu ya Kwanza iliyoongozwa na Hayati Mwl. Julius Kambarage Nyerere alikuwa mtu aliyejua kutunza na kalinda Mazingira.

Familia ya Hayati Edward Moringe Sokoine ikiwa katika Misa ya Kumbukizi ya miaka 40 ya Kifo chake, (kulia mbele) ni Balozi Joseph Sokoine na kushoto waliovaa nguo nyeupe ni wajane wa Hayati Edward Sokoine (Picha zote na Gerald Lwomile)

Akizungumza Aprili 12, 2024 mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Misa ya Kumbukizi ya Miaka 40 ya Hayati Edward Sokoine iliyofanyika Monduli Juu, wilayani Monduli mkoani Arusha. Balozi Joseph Sokoine ambaye ni mtoto wa Hayati Edward Sokoine amesema ukiwa unaingia katika Kijiji cha Enguik, Kata ya Monduli Juu utaona msitu mkubwa wa miti uliopandwa na Hayati Edward Sokoine.

Amesema msitu huo umeshamiri kijijini hapo umepandwa kwa akishirikiana na Chuo cha Misitu cha Olmotonyi kilichoko wilayani Arusha, ambapo pamoja na miti ya kigeni lakini pia walipanda miti ya asili katika eneo hilo.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa katika Misa ya Kumbukizi ya Miaka 40 ya Hayati Edward Sokoine

Akizungumzia maisha alioyoishi na wasaidizi wake, Balozi Joseph Sokoine amesema Hayati Edward Moringe Sokoine alikuwa na huruma sana, kiasi kuwa inapofika mapumziko ya mwaka ya sikukuu aliwataka wasaidizi wake kwenda kujumika na familia zao, naye alibaki akijumuika na familia yake pamoja na kuwa na shughuli nyingi za kiserikali ambazo alilazimika kuzifanyia nyumbani.

Amesema pamoja na kuwepo msitu huyo, Hayati Sokoine pia alipanda maua mbalimbali ambayo yanapendezesha nyumba yake iliyopo kijijini Enguik na huo umekuwa mfano bora kwa kizazi chake.

 Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine Mipango, Utawala na Fedha (aliyevaa miwani) ambaye pia aliwakilisha SUA katika Misa ya Kumbukizi ya miaka 40 ya Kifo cha Hayati Edward Sokoine wilayani Monduli mkoani Arusha

Kauli hiyo ya Balozi Joseph Sokoine inathibitishwa na aliyekuwa Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine Taaluma na Ushauri wa Kitalaamu Prof. Peter Gilla ambaye katika Mdahalo wa Kumbukizi ya miaka 40 ya Hayati Sokoine uliofanyika Aprili 8, 2024 katika Kampasi ya Edward Moringe Sokoine SUA alisema akiwa Chuo cha Misitu Olmotonyi na wanafunzi wenzake walishiriki kupanda miti katika msitu uliopo Enguik wilayani Monduli.

Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo SUA kilipewa jina la heshima la mwanasiasa huyo Hayati Edward Sokoine mwaka 1984, kabla ya hapo kilikuwa ni Chuo Kikuu Kishiriki cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam tangu mwaka 1970 na kilianza na Vitivo vya Kilimo, Misitu  na Tiba za Mifugo.

Picha chini ni viongozi mbalimbali kutoka Serikali, Taasisi na wananchi wakiwa katika Misa hiyo 👇











Post a Comment

0 Comments