SUAMEDIA

Wadau wa elimu SUA waendelea kuboresha mitaala

 

Na: George Joseph

Wadau mbalimbali wa elimu kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) wameendelea kupitia na kufanya mabadiliko ya mitaala ya elimu ya Chuo itakayotumika kwa ajili ya ufundishaji wa masomo mbalimbali yanayotolewa na Chuo hapo.


Baadhi ya wadau wa elimu kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) walioshiriki kupitia na kufanya mabadiliko ya mitaala ya elimu ya Chuo hicho


Akizungumza katika mkutano huo Mwenyekiti wa Kamati ya Seneti inayoshughulika na masuala ya Stadi za Awali  Dkt. Damas Philip amesema lengo la kufanya mapitio ni kuboresha kulingana na hali ya kiuchumi ili uendane na maendeleo ya taifa na pia kuzalisha wahitimu ambao wanakua na stadi bora za kufanya kazi kulingana na fani wanazo somea.

Nae Mwl. Lidya Bupilipili anayefanya kazi katika Ofisi ya Mkurugenzi wa Huduma kwa Wanafunzi ameongeza kuwa mapitio ya maboresho hayo yatasaidia kuimarisha zaidi wahitimu kulingana na uhitaji wa sasa katika jamii, na kuongeza kuwa masomo kama ya usuluhishaji wa migogoro yatasaidia kutatua migogoro mbalimbali katika jamii wanazoenda kuzihudumia.

Ameongeza kuwa mtaala mpya pia utamuwezesha mwanafunzi wa kila fani anayehitimu kuwa na uwezo wa kujiajiri  mwenyewe kuliko kutegemea ajira  Serikalini, hata hivyo amesema kuwa kwa wale watakaotaka kupata kazi Serikalini na sekta binafsi watafanya vyema katika ushindani kwenye soko la  ajira.

Mapitio hayo ya mitaala yanayoendelea  SUA ni muendelezo wa shughuli za uboreshaji wa elimu unaotekelezwa na Mradi wa Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Kiuchumi (HEET)  kwa miaka mitano na kufadhiliwa na Benki ya Dunia.





Post a Comment

0 Comments