SUAMEDIA

SUA yazindua magari matatu kurahisisha shughuli za utekelezaji wa Mradi wa HEET

 

Na: Winifrida Nicolaus

Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) katika utekelezaji wa maeneo saba ya Mradi wa Elimu ya Juu kwa Mabadiliko ya Kiuchumi (HEET) kimezindua Magari matatu, mawili aina ya Double Cabin na moja aina ya Land Cruiser Hardtop kwa lengo la kusaidia kurahisisha shughuli za mradi huo kwa ufanisi mkubwa ikiwemo ufuatiliaji wa masuala ya ujenzi.




Amebainisha hayo Dkt. Winfred Mbungu Naibu Mratibu wa Mradi wa HEET SUA wakati akizungumza na SUAMEDIA kwenye uzinduzi wa Magari hayo Kampasi ya Edward Moringe Mjini Morogoro.

Amesema wamekuwa na shughuli nyingi ambapo zingine zitaanza hivi karibuni hasa za kufuatilia mambo mengi ya ujenzi ambapo wamekuwa wakihitaji usafiri na mara nyingi wamekuwa wakitumia magari ambayo yamekuwa na shughuli zingine Chuoni hapo hivyo magari hayo yaliyozinduliwa yatarahisisha kazi kwa sababu ni mahususi zaidi kwaajili ya utekelezaji wa shughuli za Mradi.

Dkt. Mbungu amesema wanatoa shukrani kwa Fedha hizo walizozipata kupitia Mradi wa HEET pamoja na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ambazo zimewezesha kupelekwa SUA na pia kuwezesha kununua hayo magari ambapo wanatumaini yataboresha Mazingira ya watu kujifunzia pamoja na kufundishia na pia kuboresha kiwango cha wahitimu wao ambao watamaliza SUA.

Hii ni seti moja wapo lakini tuna magari mengine tunayatarajia hapo baadae ambayo yatakuwa zaidi mengine ni kwa Mafunzo kwa vitendo zaidi kwa maana ya mabasi pamoja na minbus kwaajili ya kurahisisha shughuli za mafunzo kwa vitendo lakini haya tuliyoyazindua ni zaidi kwaajili ya kufanikisha shughuli za kukimbia kufuatilia utekelezaji wa Mradi amesema”, Dkt. Mbungu.

Aidha Dkt. Mbungu  ametoa wito kwa wadau wote wakiwemo watekelezaji wa Mradi ambao ni Chuo kizima kwa ujumla kuwa washirikiane ili kuweza kutekeleza malengo ya Mradi ambao upo mahususi kwaajili ya kuinua shughuli za kitaaluma ikiwemi uboreshaji wa Mitaala, programu mbalimbali Chuoni hapo lakini pia Miundo mbinu wezeshi kwaajili kujifunzia na kufundishia ili ifikapo mwaka 2025/2026 kuwepo na mabadiliko yenye tija.






 

Post a Comment

0 Comments