Serikali ya Tanzania imeahidi kuwasomesha nje ya nchi Wahadhiri wa Vyuo Vikuu kikiwepo Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo kwa lengo la kusaidia Wahadhiri hao kutoa Elimu yenye ubora na kukabiliana na Soko la Ajira kimataifa.
![]() |
Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda akizungumza katika hafla ya Uzinduzi wa Mradi wa HEET. |
Kauli hiyo imetolewa leo Septemba
13, 2022 na Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda wakati wa
uzinduzi wa Mradi wa HEET wenye lengo la
kuboresha Elimu nchini kwa kuwapeleka Wahadhiri kusoma nchi mbalimbali ambapo
inategemewa mradi huo kunufaisha Vyuo 14 nchini.
Mradi wa HEET ambao
utatekelezwa kwa muda wa miaka mitano 2021-2026 umezinduliwa jijini Dar es
Salaam ukihusisha uwepo wa Benki ya Dunia, Wizara ya Fedha, Makamu Wakuu wa
Vyuo (Taasisi za Elimu ya Juu na Afya), Waratibu wa Mradi kutoka Taasisi
zinazonufaika pamoja na Wawakilishi wa waliopata ufadhili.
![]() |
Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknolojia Dkt. Francis Michael akitoa maagizo kwa wasimamizi wa Mradi wa HEET wakati wa Uzinduzi. |
0 Comments