Na Calvin Gwabara
Umoja wa
watengeneza bidhaa za asili Tanzania (UWABIATA) umepongeza Chuo Kikuu cha
Sokoine cha Kilimo (SUA) kupitia watafiti wake kwa namna wanavyo walea Waganga
wa tiba asili nchini na kufanya tafiti zinazoleta tija katika utoaji wao wa
huduma.
Shukrani hizo zimetolewa na Mwenyekiti wa UWABIATA Bw. Rajabu Hamisi Mbambwa wakatia akiongea na SUAMEDIA mara baada ya kumalizika kwa Mkutano wa kwanza wa kisayansi wa tiba asili nchini uliofanyika SUA Mkoani Morogoro na kuwakutanisha Waganga wa tiba asili kutoka nchi nzima,watunga sera,Wizara ya Afya na watafiti kutoka taasisi mbalimbali za utafiti nchini zinazohusiana na tiba asili.
“Matabibu
wengi wa tiba asili elimu yao sio kubwa na wengine hawakusoma kabisa lakini SUA
wametutambua na kutupokea lakini kubwa zaidi wameithamini tiba asili na kwa
muda sasa tunafanya kazi nao katika kufanya tafiti na kuboresha namna ya utengenezaji
wetu wa dawa asili kutoka kienyeji na kutengeneza kisasa kufikia viwango na
masoko ya ndani na nje” alisema Bw. Mbambwa.
“Aliongeza
wakati tupo kwenye maonesho tumepata maelezo katika banda la SUA kutoka kwa mwananfunzi
anayesoma Shahada ya Udaktari wa Falsafa katika maswala ya tiba asili, hakika
hili limetupa faraja sana kuona wasomi wanaamua kubobea katika kuifanya tiba
asili ifanye kazi kisasa badala ya kubaki na mbinu za jadi”.
Mwenyekiti
huyo wa UWABIATA ameiomba SUA kuendeleza jitihada hizo za mashirikiano ili
kuwawezesha watengeneza dawa za asili Tanzania kutengeenza bidhaa bora ambazo
zitakidhi viwango vya kimataifa na hivyo kuwezesha dawa za Tanzania kuingia
kwenye masoko ya dunia kama ambavyo dawa za nchi kama China na India
zinavyouzwa kwa wingi nchini.
Umoja wa Watengenza
Bidhaa za Asili Tanzania UWABIATA ni matokeo ya matunda ya kazi kubwa
zilizofanywa na SUA kupitia Mradi wake wa GRILL na VaSPARD inayolenga kuongeza
thamani za mazao yatokanayo na mimea dawa pamoja na kutumia teknolojia na
ubunifu katika kuongeza kipato na kuboresha Maisha kupitia mimea dawa.
CG/GL MWISHO.
0 Comments