Dar es Salaam. Hatimaye aliyekuwa meneja Shirika la Reli
Tanzania (TRC) kanda ya Dar es Salaam, Jonas Afumwisye aliyekuwa anashikiliwa
na Jeshi la Polisi ameachiwa kwa dhamana, Mwananchi linazo taarifa.
Afumwisye ameachiwa leo Agosti 31, 2022 ikiwa ni siku ya sita
tangu ashikiliwe na jeshi la Polisi Kanda maalumu ya Dar es Salaam, kutokana na
tuhuma zilizokuwa zinamkabili za kupinga tozo za miamala kwenye mitandao ya
kijamii.
Msimamo wa kupinga tozo hizo kulimsababishia, Agosti 19,
Mkurugenzi Mkuu wa TRC, Masanja Kadogosa amwandikia barua Afumwisye kumjulisha
kuhusu uamuzi wa kumfuta kazi baada ya kuthibitika kwa tuhuma zilizokuwa
zikimkabili kabla ya Agosti 24 kukamatwa na Polisi.
Taarifa za kuachiwa kwake zimethibitishwa na wakili wake Peter
Kibata huku akieleza kwamba pamoja na kuachiwa kwake wamewasilisha rufaa ya
kupinga kufutwa kazi kwa Afumwisye.
“Tumekata rufaa ya kupinga kufukuzwa kazi na TRC huko tume ya
utumishi wa umma tangu Agosti 29 mwaka huu na imepokelewa sasa tunasubiri
maelekezo ya tume namna rufaa itakavyoshughulikiwa,” amesema Kibatala
0 Comments