Na Amina Hezron
Morogoro
Mkuu wa Mkoa
wa Morogoro Mhe. Martini Shigella amempongeza Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha
Sokoine cha Kilimo (SUA) Prof. Raphael Chibunda
kwa kuandaa hafla ya futari kwa ajili ya jumuiya ya chuo pamoja na
wanazuoni ambayo itazidi kuongeza umoja, upendo na mshikamano miongoni mwao.
Akizungumza katika hafla hiyo Mhe. Shigella amesema hafla hiyo iwe fundisho kwa taasisi zingine ambazo hazijawahi kufanya jambo kama hilo ili likaongeze mshikamano katika kazi zao.
“Nawashukuru
sana Prof. Chibunda na wafanyakazi pamoja na wanazuoni wa SUA kwa kuonyesha
upendo Mwenyezi Mungu akawafanyie heri katika mambo
yenu na pale mlipotoa basi akapajazie pakaongezeke zaidi”, alisema Mhe.
Shigela.
Naye Makamu
Mkuu wa Chuo Prof. Raphael Chibunda amesema nia ya kuandaa futari hiyo ni
kuhakikisha chuo kinazidi kudumisha mshikamono uliopo baina ya Manejimenti,
wafanyakazi na wanafunzi wake.
Makamu Mkuu wa Chuo Prof. Raphael Chibunda akizungumza na wanajumuiya ya SUA kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi
Amewataka
kuzidi kumuomba Mwenyezi Mungu katika kipindi kizima cha kumalizia mfungo wa Mwezi
wa Ramadhani ili azidi kuwaongezea nguvu upendo na mshikamano miongoni mwao na
majirani wanaokizunguka chuo hicho.
Kwa upande
wake mwakilishi wa Sheikh. Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Sheikh. Selemani Lukanda amekipongeza
Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo SUA kwa kuona haja ya kuandaa hafla hiyo ya
kuonyesha umoja na udugu ambao uliasisiwa na wazee wa zamani ambao walikwisha
tangulia mbele za haki kwa kuwa pesa zilizotumika kuandaa hafla hiyo zingeweza
kutumika kufanya majukumu mengine ya chuo.
Sheikh. Selemani Lukanda akitoa salamu za Sheikh Mkuu wa mkoa wa Morogoro
“Hii ndiyo
tunu ambayo nchi yetu ya Tanzania imetunukiwa na Mwenyezi Mungu kwa kuwa mambo
kama haya ni nadra sana kuyaona katika nchi zingine kuwaona waislamu
wanajumuika na wasiowaislamu kupata futari kwa pamoja katika hali ya usalama na
amani kabisa, hivyo ni muhimu kuzidi kumuomba Mungu aendelee kutulinda na
kutusimamia amani hii iendelee kuwepo “, alisema Sheikh Lukanda.
0 Comments